Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Edmund Mndolwa akimpa zawadi Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Philip Mangula katika kongamano la chama hicho
Baadhi ya Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi pamoja na chama cha Mapinduzi wakiwa katika Kongamano la Jumuiya
Mjumbe wa kamati ya Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Ilala Abdalah Othiman (kushoto)akisalimiana na Mjumbe wa Kamati ya Siasa wilaya ya Ilala Baraka Obama katika kongamano la wazazi .
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana UVCCM Taifa Khery James akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kivukoni Sharik Choughule katika Kongamano la jumuiya Wazazi Taifa
PICHA NA HABARI HERI SHAABAN
JUMUIYA ya wazazi Chama cha Mapinduzi (CCM ) Taifa wametuma maombi kwa Mwenyekiti wa ccm Taifa Rais John Magufuli wakitaka Wabunge wa kundi la Jumuiya ya Wazazi pamoja na madiwani wachaguliwe na Baraza Kuu la Jumuiya hiyo.
Mapendekezo hayo ya ushauri kwa Rais John Magufuli yalisomwa katika hotuba na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Taifa Dkt,Edmund Mndolwa wakati wa Kongamano la kumpongeza Rais Magufuli kwa kuchaguliwa Mwenyekiti wa SADC na utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Mndolwa alisema kwa sasa Wabunge wa kundi la wazazi wawakilishi Bungeni wanachaguliwa na baraza kuu la Umoja wa Wanawake UWT wakati jumuiya ya wazazi inawajua watu wake vizuri katika kukisaidia chama.
'"Desemba 2017 ulipokuwa ukifungua Mkutano Mkuu wa Wazazi Taifa uliofanyika Dodoma ulituahidi ombi letu la kuongezewa Wabunge na Madiwani wa Viti Maalum wanaotokana na jumuiya yetu ulilipokea ukasema unagawanya viti hivyo kwa jumuiya zote tatu hivyo tunakumbusha agizo letu"alisema Mndolwa.
Mndolwa alisema mwaka 2020 ni mwaka wa uchaguzi Mkuu wa Rais,wabunge na madiwani hivyo kama jumuiya wameomba watangaziwe mapema kuwajulisha wanachama wa jumuiya ya wazazi wabunge wawili bila madiwani pengo kubwa sana.
Aidha alisema jumuiya ya wazazi ndio inajua wawakilishi wanaofaa kama watachaguliwa na jumuiya nyingine sio vizuri.
Wameshauri wagombea wote wapitie katika mchakato wa chama chao mwisho waishie katika Baraza la Wazazi Taifa kwa niaba ya mkutano mkuu.
Wakati huohuo Mndolwa alitumia nafasi hiyo kumpongeza Rais John Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC uteuzi huo unakwenda sambamba na uadilifu wako,uzalendo wako , uchapakazi na utendaji kazi wako mahili.
Pia Jumuiya ya Wazazi Taifa wamempongeza Rai s Magufuli kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM ujenzi wa barabara za juu ,ujenzi wa daraja jipya mto wami pamoja na miradi mkakati katika kujenga Tanzania ya uchumi wa viwanda.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti CCM Tanzania Bara Philip Mangula amezitaka Kamati za siasa za Chama cha Mapinduzi wawe na siri katika kupitisha majina ya wagombea wasiwe wanatoa siri za chama .
Mangula alisema wakati CCM ikielekea katika uchaguzi mwakani amezitaka kamati za siasa kufuata sheria na kanuni wawe na kifua cha ujasiri wasitoe siri za wagombea waliopitishwa na kamati ya siasa wakati wa kujadili majina.
"Chama chetu kinaelekea katika uchaguzi mkuu wa Rais wabunge na madiwani mwaka 2020 naziomba kamati za siasa zote kuacha ushabiki wa kukumbatia wagombea wakati wa mbio za kampeni bado"alisema Mangula
Post A Comment: