Mkuu wa wilaya ya Kilolo mkoa wa Iringa Asia Abdallha (pichani)amesema amepata vitisho vingi sana hata kulimwa barua na mwanasheria wa Halmashauri ya Kilolo wakati akitekeleza majukumu yake ya kupigania wananchi wa kijiji cha Magome kupata ardhi yao zaidi ya hekari 300 walizokuwa wameporwa na dalali wa kijiji .
Akizungumza jana kwenye mkutano wa hadhara kijiji cha Magome alisema kuwa kazi yake kama mwakilishi wa Rais kwa ngazi ya wilaya ni kuendelea kuwatumikia wananchi wa Kilolo tena bila kutaka malipo yoyote kwani mshahara ambao analipwa na serikali unamtosha kuwatumikia wananchi hao
Alisema sakata hilo la ardhi Zaidi ya hekari 300 ambazo mwananchi mmoja aliyefahamika kwa jina la Kisoma alitaka kuwatapeli wananchi wa kijiji hicho na kuuza kwa makampuni ya kigeni ya miti yaliyopo wilaya ya Kilolo ,lilipelekea kulimwa barua na mwanasheria wa Halmashauri ya Kilolo akimtaka kutoingilia kati kuwatetea wanyonge hao ila kesi hiyo baada ya kwenda mahakamani ushindi ulirudi kwa wananchi hao .
Kuwa alipambana kufa na kupona na hata kuhatarisha maisha yake kutoka kwa dalali huyo wakati akitekeleza wajibu wake wa kupigania haki ya wananchi iliyokuwa imeporwa na dalali huyo kwa maslahi yake binafsi .
Hivyo alitaka kuanzia sasa wawekezaji wanaofika Kilolo ni lazima kufuata taratibu za uwekezaji kwa kupitia kituo cha Taifa cha uwekezaji ama ofisi ya mkoa na wilaya sio kwenda moja kwa moja kijijini kutaka kuwatumia madalali kuchukua ardhi ya wananchi .
Mkuu huyo wa wilaya alisema ofisi yake imekuwa ikifanya kazi bega kwa bega na ofisi ya mkoa wa Iringa chini ya mkuu wa mkoa Alli Hapi na katibu tawala Happines Seneda kuona wananchi wa wilaya ya Kilolo wanafanya shughuli zao kwa amani na utulivu na kero mbali mbali zinapojitokeza zinashughulikiwa haraka
Kwa upande wake mkazi wa kijiji cha Magome mzee Amon Mtagi(84) ambae alisaidiwa na mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdallah kupata ardhi yake aliyoporwa na mtumishi wa umma mstaafu asema kama ingekuwa inawezekana Mungu aanze kumchukua yeye kwanza mkuu huyo wa wilaya abaki aendelee kumsaidia Rais Dkt John Magufuli kutetea wanyonge .
“Mimi na wananchi wenzangu wa kijiji hiki cha Magome tuliumizwa sana na uporaji wa ardhi aliotaka kuufanya msaafu huyu wa umma ambae alichukua sehemu kubwa ya ardhi ya kijiji na sisi wanyonge kukosa ardhi tulizunguka sana kwa viongozi mbali mbali na wakati huo mkuu wa mkoa wa sasa Alli Hapi alikuwa hajafika ila hatukusikilizwa ila binafsi nakushukuru sana mama Asia Abdallah wewe ulisimama mbele kututetea na tumepata haki zetu “ alisema mzee huyo huku akitokwa na machozi ya furaha
Kuwa amani ya wananchi wa kiiji hicho ambayo ilitaka kutoweka kwa wananchi kutaka kumvamia mstaafu huyo kwa mapanga ilirejea na Imani yao kwa serikali ya Rais Dkt Magufuli imezidi kuongezeka Zaidi baada ya kutetewa kupata ardhi yao waliyokuwa wametapeliwa na mwananchi huyo mmoja .
“Mkuu wa wilaya ya Kilolo wewe umekuwa ni mkombozi wetu na mtetezi mkubwa wa wanyonge katika wilaya hii ya Kilolo nakumbuka siku ile nilipokuja kufuatilia ardhi yangu baada ya kuzunguka sana sikuwa tena na uwezo wa kifedha hata kurudi nyumbani ila ulinisaidia mimi na wenzangu kupata ardhi yetu hekari Zaidi ya 300 zilizoporwa pia ulisaidia fedha za kijikimu na kuweza kurudi nyumbani sina cha kukulipa kwa niaba ya wenzangu ila nasema kwa kuwa mimi umri wangu umekwenda na natamani sana kama inawezekana hata leo Mungu aanze kunichukua mimi na wewe mkuu wa wilaya uendelee kubaki kutetea wananchi wanyonge kama anavyofanya Rais wetu mpendwa Dkt John Pombe Magufuli “ alisema mzee Amon Matagi
Post A Comment: