Na  Avitus Benedicto Kyaruzi, Kagera
Wananchi  mkoani Kagera wametakiwa kufuata taratibu za kuwapokea wageni kutoka nchi jirani za Uganda Rwanda Burundi na Kenya na sio kuwa pokea nakuwatunza kinyemera katika maeneo yao na kuwapa makazi bila kufuata sheria za nchi. 

Hayo yamebainishwa na mkuu wa idara ya uhamiaji nchini Tanzaia  Anna Makakala wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za mkuu wa mkoa huo akiwa katika ziara ya kikazi itakayodu kwa siku tatu hapa mkoani kagera  ambapo kwasiku hizo tatu atazungukia wilaya zote za mkoa wa kagera pamoja na kuzungukia mipaka ya mkoa wa kagera  kwa upande wa nchi jirani. 

Makakala ameongeza kuwa Wageni kutoka nchi mbalimbali jirani waingie nchini kwa kufuata taratibu maalumu na kuwa tahadharisha wananchi mkoani hapa kuwa hatakaye bainika akimkaribisha mgeni pasipo kufuata sheria na kanuni  za nchi hatua kali za kisheria na hadhabu kali ya kifungo cha miaka 20 au kutozwa faini ya milioni 20 zita chukuliwa dhidi yake. 

Naye mkuu wa mkoa Kagera brigedia Generali  Marco Gaguti  amesema kuwa mkoa wa Kagera hupo salama na hakuna wa amihaji haramu katika mkoa huu ni kutokana na kazi  nzuri zinazofanywa na idara ya uhamiaji , na kamati ya ulinzi na usalama  ya mkoa kwa kushirikiana na wananchi.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: