Spika Job Ndugai ameagiza Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), afike mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge leo saa 8:00 mchana kujibu tuhuma zinazomkabili za kulidharau na kulidhalilisha Bunge

Spika amesema kuwa Bunge analoliongoza si dhaifu na yeyote atayeingia kwenye 18 zao anaalikwa kwenye mchezo huo.

Aidha, asemema huwa Mbunge huyo wa Arusha Mjini ana msongo wa mawazo kwani tangu aingie Bungeni, amekopa Tsh. Milioni 644.

 
“Yapo mambo ambayo hawasemi wacha tuseme kidogo amekopa Sh 644 milioni…Sasa hivi ameshalipa lipa zimefika Sh 419 milioni huu ni msongo wa mawazo ndio maana anafika mahali anajilipua tu na kadhalika,”amesema.

Katika hatua nyingine amemfukuza ndani ya Ukumbi wa Bunge, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko(CHADEMA) baada ya kupiga kelele kumpinga kiongozi huyo kutaja deni la Lema.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: