Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Kilakala, akizungumza kwenye uzinduzi wa Dar es Salaamya Kijani. Hlafa hiyo ilifanyika Chuo Kikuu Kishirikishi cha Elimu Dar es Salaam (DUCE),  na kuhudhuhuriwa na vijana wote wa Mkoa wa Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa UVCCM, Mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Kilakala (kushoto), akiwa na mgeni rasmi katika uzinduzi wa Dar es Salaam ya Kijani, Katibu Mkuu wa UVCCM Mwal. Raymond Mwangwala (kulia).
 Baadhi ya Vijana wa CCM wakiwa kwenye uzinduzi wa Dar es Salaam ya Kijani

Na MWANDISHI WETU
-DAR ES SALAAM
UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Mkoa wa Dar es Salaam, umezindua kampeni ya ‘Dar es Salaam ya Kijani’ ikiwa na lengo la kurudisha mitaa na majimbo yaliyokwenda upinzani.
Kampeni hiyo inalenga kuweka mikakati kwa kuanzia ngazi za jumuiya zote za mkoa huo, kuanza kujipanga kuelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu pamoja na Uchaguzi Mkuu  mwaka 2020.
Akizugumza katika uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika Chuo Kikuu Kishirikishi cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Kilakala, amesema kuwa kampeni hiyo itachochea ustawi zaidi wa CCM katika Mkoa wa Dar es Salaam na kuzidi kukita mizizi katika ngazi zote kuanzia mkoa hadi majimbo, wilaya hadi kata, na matawi hadi mitaa.
“Leo tunazindua kampeni yetu ya “Dar es Salaam ya Kijani kuelekea serikali za mitaa 2019”, kampeni kabambe kwa ajili ya kuirejeshea CCM mitaa iliyopotea katika uchaguzi uliopita ambayo kwayo itatusaidia kupata ushindi mkubwa kimkoa katika Uchaguzi Mkuu wa 2020 wa udiwani, ubunge na urais.
“Sote tu-mashuhuda kwamba katika uchaguzi uliopita wa 2014 wa Serikali za Mitaa na ule Mkuu wa 2015 tulipoteza baadhi ya mitaa, kata na majimbo yaliyokuwa yakishikiliwa na CCM.
“Na sababu za kupoteza huko zinajulikana, sina haja ya kuzirejea sasa. Hivyo sisi vijana wa CCM tunatambua kuwa ndiyo damu na roho ya chama chetu, na kwamba tunao wajibu wa asili wa kusafisha njia katika kutimiza malengo ya uwepo wa vyama vya siasa kikatiba ya kushika dola,” amesema Kilakala
Mwenyekiti huyo wa UVCCM, amesema kuwa CCM inahitaji ushindi mkubwa kwa kuweka mikakati ya awali kwa kuwahusisha wanachama wa chama hicho wa ngazi zote.
“Kampeni yetu hii itashuka katika wilaya, kata na matawi yote katika Mkoa wetu ili kuwa na ufahamu wa pamoja na kuhakikisha kila Kijana wa UVCCM anawajibika ipasavyo kuhakikisha falsafa ya Dar es Salaam ya kijani yaani Dar es Salaam ya CCM inaenea kwa wanachama na wananchi ili ikifika wakati wa uchaguzi tuvune wapiga kura wa kutosha.
 “Nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sitatoa pongezi zangu za dhati kwa niaba ya Mkoa wa Dar es Salaam kwa Mwenyekiti wetu wa CCM Taifa na Rais Dk. John Magufuli kwa kutuongoza vyema kupitia Serikali yetu ya CCM katika jukumu la kutatua changamoto za watanzania na kuwaletea maendeleo.
“Tumejionea dhahiri shahiri namna yale yaliyochelewa yakiwahishwa, yaliyoshindikana yakiwezekana, magumu yakiwa mepesi, yaliyokwama yakikwamuliwa,”amesema Kilakala
Kwa upande wake mgeni rasmi, Katibu Mkuu wa UVCCM, Mwal. Raymond Mwangwala, amesema ameridhishwa na kasi kubwa inayofanywa na vijana wa Dar es Salaam ya kuhakikisha chama kinapata heshima katika chaguzi zote.
“Leo ninachokiona hapa, hii ndiyo UVCCM ninayoijua na sina shaka na uongozi wa mkoa kwani unafanyakazi kubwa na nzuri, ninachoweza kusema kwenu ninawaomba sana vijana tukilinde chama na kuhakikisha tunapata ushindi katika chaguzi zote.
“Na ikiwezekana si waachieni (upinzani) asimilia mbili tu ya mitaa na pindi ikibidi hata hakikisheni tunachukua asilimia yote 100. Vijana tushikamane na tulinde heshima ya chama chetu,” amesema Mwal. Mwangwala
Mwisho
Share To:

Post A Comment: