Hali si shwari tena ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini, baada ya jana diwani mwingine wa chama hicho, Ndg. Baraka Saimon kuandika barua ya kujiuzulu udiwani na kujiunga na CCM.

Asubuhi hii ya leo Diwani mwingine wa kata ya Kiutu katika Halmashauri ya Arusha ( Arusha Dc ) Ndg.Zephania Sirikwa wa (Chadema) na Aliyekuwa Mwenyekiti wa Maadili katika Halmashauri hiyo amejiuzulu uanachama na udiwani na kutangaza kujiunga na ccm kwa kile alichoeleza kuwa amefanya hivyo ili kuunga mkono juhudi za Mh.Rais Magufuli.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: