Simba na Yanga zinaweza kujikuta zinakutana mwaka huu kwa mara ya tatu mfulilizo lakini safari hii ikiwa ni katika michuano ya  SportPesa Super Cup.

Michuano hiyo inafanyika jijini Nairobi, Kenya na itakutanisha timu nane kutoka Tanzania na nne za wenyeji Kenya.

Michuano ya  SportPesa Super Cup inaanza Juni 3 hadi Juni 10 na Simba wataanza Sharks ya Kenya wakati Yanga baadaye watakuwa uwanjani dhidi ya Homeboyz.

Kama kila timu itashindana, uwezekano wa kukutana ni asilimia kubwa na kila mmoja atalazimija kujiweka vizuri mapema kabisa.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: