Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akitoa hotuba ya kufunga kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara mjini Dodoma. 
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akitoa hotuba ya kufunga kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara mjini Dodoma. 


 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akijadiliana jambo na Naibu Katibu Mkuu (ELIMU) Ofisi ya Rais TAMISEMI, Tixon Nzunda wakati wa kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara mjini Dodoma.


 Naibu Katibu Mkuu (ELIMU) Ofisi ya Rais TAMISEMI, Tixon Nzunda akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi wakati wa kikai kazi kilichofungwa jana cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara mjini Dodoma.


 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akitoa hotuba ya kufunga kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara mjini Dodoma. 
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Elimu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Paulina Mkwama akitoa utambulisho wa wageni waalikwa wakati wa kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara mjini Dodoma.
..............................................................................
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amefunga kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara ambapo amewaasa washiriki hao kutumia fedha za Serikali kwa kufuata sheria.

Mheshimiwa Ndalichako alisema Wizara ya Elimu itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Rais,TAMISEMI kwa kuwaadhibu wale wote wanaoenda kinyume na matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Elimu bila ya kuzingatia sheriaa na miongozo ya utekelezaji wake.

“Wizara ya Elimu pamoja na Ofisi ya RAis TAMISEMI itawachukulia hatua Wale wote wataokula fedha za miradi na hawatopelekewa pesa za miradi mingine hadi wakamilishe miradi ambayo haijakamilika na kutoa mchanganua wa matumizi yake,”Amesema

Ndalichako alihamasisha uzingatiaji wa taratibu za fedha kwani Viongozi wa ngazi ya juu hususani Mawaziri wamekua wakijibu tuhuma za ubadhilifu wa fedha kwa wakaguzi wakati hawakuchukua fedha hizo.

“Wengine mpaka leo miradi ya 2016 haijakamilika kutokana na ubadhilifu wa fedha. hivyo serikali haita wavumilia hata kidogo,” Alisema Ndalichako.

Katika hatua nyingine, Ndalichako amewataka Wataalam wa Elimu kutoa taarifa kwa wakati na kama kuna mambo hayaendi sawa katika Halmashauri zao, Viongozi wajuu waweze kutoa maamuzi sahihi na kwa wakati ikiwa ni pamoja na takwimu sahihi.

“toeni taarifa kwa wakati, andikeni ripoti kwa wakati, na hakikisheni matumizi yenu yanazingatia miongozo na taratibu za fedha. Muwe waungwana, kwani muungwana ni kutenda”


Alizungumzia pia suala la maudhurio shuleni na watoto kuacha shule kabla ya kumaliza mzunguko
kwani kwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2016 unaonesha bado kunatatizo la mdondoko wa wanafunzi na hapa amewataka Wasimamizi wa Sekta ya Elimu kuwa makini kufuatilia na kutoa taarifa kwa mamlaka husika ili kusaidia watoto.

Aliagiza maafisa Elimu Mkoa kuchagua wanafunzi kulingana na idadi ya madarasa kwani watoto wamekua wakilundikana kwenye darasa moja wanafunzi zaidi ya 200 wakati shule husika ina uwezo wa kupokea wanafunzi wa mkondo mmoja (wanafunzi 40).

Aliagiza Shule zote za kidato cha tano ambazo hazijasajiliwa zikaguliwe ambazo zimekidhi viwango basi zisajiliwe na zipokee wanafunzi wa kidato cha tano kwani Maafisa Elimu wamekua wakipangia wanafunzi shule ambazo hazijasajiliwe na hapa amewapa miezi mitatu watatue tatizo hili la kidato cha tano na zile shule zilizolundika wananfunzi kwamba baada ya hapo hatua nyingine zitachukuliwa dhidi yao.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi kabla ya kufunga kikao kazi hicho, Naibu Katibu Mkuu (ELIMU)
Ofisi ya Rais TAMISEMI, Tixon Nzunda alisema mambo mbalimbali ambayo yalijadiliwa kwenye kikao hicho ikiwa ni pamoja na upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi, kilimo, ufundi na biashara, uhaba wa vitendea kazi kwa maofisa elimu hasa usafiri pamoja na utoaji motisha kwa walimu ili kuongeza ufanisi mashuleni.

Pia alisema katika kikao kazi, kila mmoja amepewa jukumu la kutekeleza ikiwa ni pamoja na usalama wa watoto.

“Kila mmoja katika kikao hiki amepewa jukumu la kufuatilia miradi kwa ukaribu, kusimamia taaluma na usalama wa watoto wawapo mashulen” Alisema

kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara kimedumu kwa siku mbili na matarajio ni kwamba kuendelea kuboresha sekta ya elimu nchini hususani masuala ya kitaaluma.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: