MANCHESTER United inatarajiwa kuwa mwe­nyeji wa Liverpool, ke­sho Jumamosi kwenye Uwanja wa Old Trafford, mchezo huo ni mkubwa na unasubiri­wa kwa hamu.

Kuelekea mtanange huo, gumzo kubwa ni juu ya uwezo wa kiungo mshambuliaji wa Liverpool, Mo­hamed Salah ambapo mashabiki wa Unit­ed wameanza kupata hofu kuhusu mchezaji ambaye atamzuia.

Kawaida Salah amekuwa akipangwa kushambulia akitokea kulia, kwa aina ya ulinzi wa United beki wa kushoto am­baye atatakiwa kukutana naye ni Ashley Young au Luke Shaw, sasa hapo ndipo patamu, imeibuka hoja juu ya nani mwe­nye uwezo kati yao anayeweza kumficha Salah.

Mchezo uliopita timu hizo zilipoku­tanaa ulimalizika kwa suluhu, huku Mar­teo Darmian akipangwa kucheza beki wa kushoto, kwa sasa beki huyo siyo chaguo la kwanza la Kocha Jose Mour­inho.

Kutokana na ubora wa Salah kufun­ga, mashabiki wa United kutoka mataifa mbalimbali wamepaza sauti wakitoa maoni kuwa ni bora akaanza Shaw kwa kuwa ni beki halisi wa kushoto na hata­takiwa kupanda mara kwa mara, huku wakidai Young ambaye ndiye anay­etumika mara nyingi siyo beki halisi mch­ezo uliopita United ilicheza mbinu y a ku­zuia zaidi ki­tendo amba­cho kilimkera Kocha wa Liver­poo, Jurgen Klopp. Kwa sasa United haita­rajiwi kuendeleza staili hiyo kwa kuwa inahitaji ushindi na ipo nyum­bani.

Liverpool ina kasi kubwa ya kufunga ma­bao lakini imekuwa ikiruhusu kufungwa mabao mengi pia tofauti na United ambayo im­ekuwa ngumu kufungika hasa inapokuwa nyum­bami,Young ni winga lakini amekuwa aki­tumika kama mlinzi wa kushoto.

Mbali na Salah mas­taa wengine wa Liverpool ambao wata­takiwa ku­chungwa ni Sadio Mane na Roberto Firmino ambao wamekuwa na kasi kubwa ya kufunga hivi karibuni.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: