Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi ya Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Jaji Mstaafu
Thomas Miyaho ametangaza kuwa, Tanzania imeanza kupokea makundi makubwa
ya watalii kutoka nchi ya Israel. Ujio huu ni matokeo ya juhudi
zinazofanywa na Wadau wa utalii wa Tanzania wakishirikiana na Ubalozi wa
Tanzania nchini Israel.
Jaji
Mihayo ameyasema hayo wakati akiongea kwenye mkutano na waandishi wa
habari uliofanyika tarehe 31/7/2021 katika ofisi za TTB Makao Makuu
zilizopo jijini Dar es Salaam. Jumla ya watalii 700 wanatarajia kuja
Tanzania katika makundi matano tofauti na kila kundi litakuwa nchini kwa
muda wa siku Saba (7).
Jaji
Mihayo amesema kundi la kwanza la watalii 150 linatarajia kuwasili
nchini tarehe 2/8/2021, kundi la pili litakuwa na watalii 200 litafika
nchini Tanzania tarehe 9/8/2021, kundi la tatu la watalii 150 litawasili
tarehe 10/8/2021 na kundi la mwisho litaingia nchini tarehe 17/8/2021,
watalii hawa watatembelea vivutio vya Tanzania Bara na Visiwa vya
Zanzibar.
“
Ujio wa makundi haya ya watalii ni ishara kuwa Tanzania inaaminika kuwa
katika maeneo yote ya vivutio vya utalii, Watoa huduma wanazingatia
vigezo vilivyowekwa na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na
Watoto pamoja na Shirika la Afya Duniani za kuchukuwa tahadhali dhidi ya
maambukizi ya virusi vya UVIKO -19, ambapo tunahakikisha kwamba Watalii
wanapokuja Tanzania wanatembelea vivutio vyetu na wanarudi nchini kwao
wakiwa salama”
Aidha,
“Tunaupongeza Ubalozi wa Tanzania nchini Israel kwa kushirikiana na
kampuni ya utalii ya Excellent Guide, Tours and Safaris kufanikisha
kuleta makundi haya makubwa ya watalii. TTB inaendelea kushirikiana na
Ofisi za Balozi za Tanzania zilizopo katika nchi mbalimbali duniani na
Wadau wa utalii wa Tanzania kushwishi mawakala wakubwa kuleta watalii
Tanzania”. alisema Jaji Mihayo.
Takwimu
zinaonyesha kuwa mwaka 2019 Tanzania ilipokea watalii 16,348 kutoka
Israel, mwaka 2020 idadi ya watalii imeshuka kutokana janga la UVIKO-19
na kufikia 6,889.
Post A Comment: