Na Calvin Gwabara, Morogoro.
KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021 Luteni Josephine Mwambashi ameupongeza uongozi na Mmiliki wa Chuo Cha Afya Hermagis kwa kusaidia kuwezeshamvijana wa Kitanzania kupata Elimu ya Famasia hasa utengenezaji wa dawa na kujiajiri.
Pongezi hizo amezitoa wakati akizindua Jengo na Maabara ya kisasa (Compound Lab) ya chuo hicho kilichopo wilayani Mvomero mkoani Morogoro.
"Napongeza jitihada hizi kubwa zilizofanywa na wenzetu wa sekta binafsi kuanzisha chuo hiki muhimu kinachozalisha wataalamu wa famasia nchini kwetu maana mambo haya yalikuwa ya afanywa nje ya nchi ndio unaoana dawa zinaletwa nchini lakini sasa kupitia sayansi na teknolojia tunaona na sisi tuna uwezo was kuzalisha sawa hapahapa kupitia wataalamu wetu hii ni hatua kubwa na sasa nitamke kuwa mwenye wa uhuru unazindua Maabara hii" alieleza Mwambashi.
Akitoa taarifa ya Mradi huo wa ujenzi wa Maabara mkuu wa chuo hicho Benedict Lugarisha alisema kupitia maabara hiyo ya kisasa imewezesha wanafunzi kusoma kwa vitendo lakini pia kuzalisha madawa mbalimbali kama vile sabuni na vitakasa mikono yaani Sanitizer.
"Mhe. Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021 jengo hili limeshakamilika na linavifaa vyote muhimu vinavyohitajika kwaajili ya Wanafunzi kujifunza na lina miundombinu yote muhimu hivyo tunayo heshima kubwa kukukaribisha uweze kulitembelea, kuona namna wanafunzi wetu wanavyolitumia na vifaa vyake na kisha utuzindulie jengo hili" alisema Lugarisha.
Akizungumza mara baada ya uzinduzi huo Askofu Dkt. Owdenburg Mosses amepongeza ushirikiano mkubwa ambao Serikali ya Tanzania unautoa kwa sekta binafsi katika kuanzisha Vyuo vya Afya na huduma zingine na hivyo kuwezesha kuongeza ufanisi wa wataalamu katika utoaji wa huduma.
Alisema afya ni suala nyeti na muhimu kwa maendeleo watu na taifa lolote lile Duniani hivyo chuo hicho kitasaidia kupata wataalamu wengi ambao watakwenda kusaidia jamii na taifa katika kutoa huduma sahihi za afya zinazozingatia taratibu na kanuni zinazowaongoza.
"Tunajua sote kuwa huko mtaani karibu nchi nzima kuna vyuo vingi lakini wengi wao ni wajanjawajanja tu kwenye utoaji wa taaluma kwa watoto wetu hivyo kuwepo kwa chuo chenye miundombinu bora na ushahdi tumeuona kwa wanafunzi wenyewe wanavyotengeneza madawa mbalimbali vizuri wakitoka hapa hawawezi kusubiria ajira bali wanakwenda kujiajiri wenyewe" alisema Askofu Mosses.
Mkurugenzi wa chuo hicho Prof. Robinson Mdegela ameishukuru Serikali ya Mkoa wa Morogoro, Wilaya ya Mvomero na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa kukubali mwenge kumulika kwenye Chuo hicho na kuahidi kuhakikisha wanaendelea kupunguza uhaba wa Wafamasia nchini hasa kutokana na umuhimu wa kada hiyo ya afya.
" Sisi hatufundishi tuu watoto kupata elimu na vyeti bali tumejikita kwenye kufundisha vya vitendo ili kila mhitimu wa Chuo chetu akitoka hapa aende kujiajiri kwenye kutengeneza madawa au akaajiriwe kwenye maeneo ambayo yana uhitaji wa Kada ya Famasia kwakuwa watakuwa wahitimu wa tofauti kutokana na Elimu bora waliyoipata hapa" alisisiza Prof. Mdegela.
Alisema kwa sasa Chuo kinatoa Mafunzo ya Famasia kwa ngazi ya Astashahada (Certificate) na Stashahada (Diploma) kwa wanafunzi wayne ufaulu wa kuanzia alama "D" kwenye masomo ya Kemia na Baiolojia na kina mpango wa kuongeza kozi nyingine muhimu ambazo sina soko kubwa la ajira kwa wahitimu na mchango mkubwa kwa taifa.
Akielezea mikakati ya chuo hicho cha Afya Hermagis, Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Prof. Yonica Ngaga alisema ni kuhakikisha wanasimamia ubora wa elimu itolewayo Chuoni hapo ili ibaki kuwa ya vitendo na kuzalisha Wahitimu watakaokuwa na mchango kwa jamii hasa kwenye sekta muhimu ya afya.
" Naomba nitumie nafasi hii kuwa shauri Wazazi, Walezi na vijana wenye sifa za kujiunga na Chuo hiki wajiunge maana hawatajutia kusoma au kumsomesha mtoto kwenye Chuo huki, Tunasomesha watoto wetu ili wapate kazi za kufanya kwa kuajiriwa au kujiajiri hivyo hapa ni mahali sahihi na mimi watoto wangu wasingekuwa wamemaliza Ngazi za juu ningewaleta hapa maana ninauhakika hatokosa kazi za kufanya" alisema Prof. Ngaga.
Alisisitiza kuwa wao kama bodi ya chuo wanataka mwanafunzi anayetoka chuo hicho kama ni mfamasia awe na Elimu ya nadharia na vitendo na aweze kutengeneza baadhi ya dawa kwenye jamii na ajipatie fedha kupitia mtaji mdogo tu kulingana na uwezo wake au uwezo wa mzazi.
Mwenge wa Uhuru mwaka 2021 unaendelea na ziara yake Mkoani Morogoro ambapo leo unepokelewa kwenye Wilaya ya Mvomero kutoka Wilaya ya Kilombero ambapo unafungua miradi mbalimbali ya maendeleo ya kusambaza ujumbe wa mwenge kitaifa kwa mwaka huu unaosema " TEHAMA ni Msingi wa Taifa endelevu, Itumie kwa usahihi na uwajibikaji".
Post A Comment: