Watu
saba wanashikiliwa kwa Mahojiano na jeshi la polisi Mkoani geita
kufuatia Matukio mfululizo ya Moto uliounguza Madarasa na vifaa vya
wanafunzi katika shule ya sekondari ya geita GESECO Iliyopo mkoani humo.
Akizungumza
wakati akikabidhi baadhi ya vifaa vya wanafunzi vilivyoathirika kwa la
janga la moto huo shuleni apo mkuu wa mkoa wa geita Rosemary Senyamule
amesema wanaoshikiliwa ni wanafunzi watatu wa shule hiyo pamoja walinzi
wanne waliokuwa wanalinda shule hiyo
Sambamba
na serikali ya mkoa wa geita kufanikiwa kukabidhi magodoro 240 ,
masanduku 240 pamoja na madaftari kwa wanafunzi wa shule hiyo RC
Rosemary Senyamule amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kusadia
ukarabati wa majengo yaliharibiwa vibaya na janga hilo la moto
Post A Comment: