Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akizungumza na Watendaji na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba jana, wakati akikagua jengo la maabara ya Hospitali ya wilaya iliyopo Old Kiomboi katika ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge, akisisitiza jambo wakati akizungumza na Watendaji na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba jana.
Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula, akisoma taarifa ya miradi mbalimbali ya maendeleo ya wilaya hiyo.

Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Baadhi ya watumishi wa Wilaya ya Iramba wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Makofi yakipigwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba,  Innocent Msengi akizungumza kwenye kikao hicho.
Dkt.Mahenge (katikati) akipokea taarifa ya ujenzi wa Maabara ya Hospitali ya Wilaya ya Iramba kutoka kwa Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Hussein Sepako (kushoto)  wakati alipofika kuona maendeleo ya ujenzi huo. 
Baadhi ya wauguzi wa hospitali hiyo wakiwa nje wakati wa ziara hiyo.
Mhasibu wa mapato wa wilaya hiyo, Optatusy Ottolikiliwike, akitoa maelezo ya ukusanyaji wa mapato kwenye mnada wa Igumo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akizungumza na wananchi alipotembelea Mnada wa Igumo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula.
Mkazi wa Iramba, Lutha Nathaniel, akimpongeza mkuu wa mkoa kwa kufanya ziara katika wilaya hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akizungumza na  Mjasiriamali  alipotembelea Mnada wa Igumo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akizungumza na watendaji wa wilaya hiyo  alipotembelea Mnada wa Igumo. Kulia ni Askari Polisi wakiimarisha ulinzi eneo hilo. Katikati ni Mkurugenzi wa Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge, akipata maelezo ya Mradi wa Maji uliopo Kijiji cha Kyalosangi Kinampanda..

 Meneja wa Wakala wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASAWilaya ya IrambaMhandisi Ezra Mwacha, akitoa taarifa ya mradi huo kwa mkuu wa mkoa.

Mwonekano wa tenki la maji la mradi huo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge, akiagana na Watendaji na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba baada ya kumaliza ziara yake hiyo.

 

Na Dotto Mwaibale, Singida 

MKUUwa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge amewataka watendaji wa halmashauri kusimamia ipasavyo vyanzo vya mapato vilivyopo kwenye maeneo yao.

Mahenge alitoa agizo hilo jana wilayani Iramba mkoani hapa katika muendelezo wa ziara zake za kutembelea halmashauri zote kwa ajili ya kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na watumishi, watendaji na wananchi.

Alisema anataka viongozi hao hasa watendaji kujua kuwa kupata mapato makubwa sio lazima kuwa na vyanzo vikubwa kama madini na miradi ya mashamba bali ni  hivihivi vidogo vilivyopo ambapo vikisimamiwa vizuri vitazifanya  halmashauri kupata mapato yakutosha.

"Nataka watendaji na viongozi wenzangu wajue kwamba mnada ni chanzo kizuri sana cha mapato hivyo kitiliwe maanani, kuna dhana kuwa ili kupata mapato makubwa ni lazima kuwepo na miradi mikubwa na vitu vingine vinavyofanana na hivyo hapana hivi hivi vidogo vikisimamiwa vitafanya mambo makubwa," alisema Mahenge.

Dkt.Mahenge alisema katika ziara yake hiyo wilayani humo aliamua kutembelea mnada ikiwa ni chanzo mojawapo cha mapato ambacho kimsingi kinajumuisha watu wengi sana.

Aliyata makundi hayo ya watu kuwa ni wachoma nyama, wauza nguo,mifugo na makundi mengine na kuwa alichojifunza ni kutokuwepo kwa usimamizi mzuri wa ukusanyaji wa mapato licha ya kuwepo kwa makundi hayo.

" Nimejifunza hatuna usimamizi mzuri na kuwa chanzo hicho  kipokipo tu kwa sababu hayupo mtu anaye hakiki upatikanaji wa mapato kama yamepanda au kushuka na kwanini makusanyo yana kuwa yale yale kila wakati.

Alisema katika minada aliyoitembelea amebaini kutokuwepo kwa utaratibu wa kuwa sajili wanunuzi wa mifugo kwenye eneo moja badala yake kila mtu anafanya kivyake jambo linalosababisha upotevu wa mapato.

Dkt. Mahenge alisema kukosekana kwa usimamizi mzuri wa mapato katika maeneo hayo kunasababishwa na baadhi ya watendaji wa serikali ambao sio waaminifu ambao wamechangia kutotumika kwa maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za ununuzi na uuzaji wa mifugo na badala yake kwa kushirikiana na wanunuzi hao wamekuwa wakifanyia shughuli hizo nje ya maeneo hayo.

Aidha alisema jambo kubwa analolihitaji ni usimamizi mzuri wa ukusanyaji wa mapato kwenye mifugo na kwa wafanyabiashara wengine ambao wanafanya shughuli za kibiashara kwenye eneo hilo la mnada ambao wengi wao hawana vitambulisho vya ujasiriamali hivyo ametaka kuongezwa kasi ya utoaji wa vitambulisho hivyo kwani wananchi wako tayari lakini hawajapa fursa ya kuvipata. 

Alizitaka timu za ukusanyaji wa mapato za halmashauri kunapokuwa na minada kwenda kujionea ukusanyaji wa mapato badala ya kumuachia mtu mmoja ambaye anaweza kurubuniwa na kusababisha upotevu wa mapato. 

Dkt.Mahenge katika ziara yake alitembelea na kukagua ujenzi wa jengo la maabara hospitali ya wilaya ambapo hakuridhishwa na gharama halisi zilizotumika kwa ujenzi huu kuanzia msingi hadi hatua ya linta na kumwagiza mkuu wa wilaya hiyo kufanya uchunguzi.

Aidha alikagua ukusanyaji wa mapato katika Mnada wa Igumo na mradi wa maji uliopo Kijiji cha Kyalosangi.

Share To:

Post A Comment: