Kaimu Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida,  Frederick  Ndahani, akihutubia katika  Mahafali ya vijana waliohitimu mafunzo ya Ufundi Stadi katika fani za ushonaji, uashi, useremala, ufundi pikipiki, ususi ,urembo na uhunzi  yaliyofanyika  Kijiji Cha Iseke wilayani Ikungi kwa ufadhili wa Shirika lisilo la Kiserikali la SEMA lenye makao yake makuu mkoani Singida kwa ushirikiano wa Shirika la STROMME.


Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la SEMA Peter Lissu, akiwa kwenye mahafali hayo.


Kaimu Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida,  Frederick  Ndahani, akiangalia kazi za wahitimu wa mafunzo ya ufundi wa Kata ya Iseke, na Muhintiri, Ikungi mkoani Singida.

Kaimu Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida  Frederick  Ndahani, akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu na viongozi mbalimbali.
Kaimu Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida  Frederick  Ndahani, akikabidhi vyeti.
Kaimu Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida  Frederick  Ndahani, akiangalia kazi za wahitimu wa mafunzo ya ufundi wa Kata ya Iseke, na Muhintiri, wilayani Ikungi mkoani Singida.
Kaimu Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida  Frederick  Ndahani, akiangalia kazi za wahitimu wa mafunzo ya ufundi wa Kata ya Iseke na Muhintiri wilayani Ikungi mkoani Singida.

Kaimu Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida  Frederick  Ndahani, akikabidhi vyeti kwa wahitimu.

Kaimu Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida  Frederick  Ndahani, akikabidhi vyeti.

Kaimu Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida  Frederick  Ndahani, akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu na viongozi mbalimbali.
 


Na Dotto Mwaibale, Singida.


KAIMU Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida,  Frederick  Ndahani amezitaka Halmashauri za Vijiji na Mitaa Mkoani Singida kutenga maeneo kwa ajili ya shughuli za Vijana.

Ndahani ambaye alikuwa mgeni rasmi ameyasema hayo katika  Mahafali ya vijana wa Kata za Iseke na Muhintiri waliohitimu mafunzo ya Ufundi Stadi katika fani za ushonaji, uashi, useremala, ufundi pikipiki, ususi ,urembo na uhunzi  yaliyofanyika  Kijiji cha Iseke wilayani Ikungi kwa ufadhili wa Shirika lisilo la Kiserikali la SEMA lenye makao yake makuu mkoani Singida kwa ushirikiano wa Shirika la STROMME.

Alisema Serikali ilishatoa mwongozo kwa kila halmashauri kutenga maeneo ya shughuli za vijana lakini unakuta baadhi ya viongozi wanatoa taarifa kuwa maeneo yametengwa lakini ukifuatilia unakuta hakuna hata eneo lilitengwa kwa shughuli za Vijana.

" Jambo hili siyo sawa tunakuwa hatuwatendei haki vijana wetu nawaomba viongozi wa kamati ya maendeleo ya kata kuhakikisha suala hili la kutenga maeneo hayo linatekelezwa kwa vitendo." alisema Ndahani.

Aidha Ndahani aliwataka vijana kutumia umeme vijijini ulioletwa na Serikali kwa ajili ya kuendeleza ujuzi na kufungua Shughuli za kimaendeleo katika Vijiji vyao badala ya kukimbilia mjini.

Kwa upende wao vijana kupitia risala yao wameomba kupatiwa mikopo ili ujuzi walionao waweze kuuendeleza na kuutumia kwa ajili ya kujikwamua na umasikini.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la SEMA Peter Lissu ameishukuu Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuonesha ushirikiano na mashirika yasiyo ya Kiserikali na kuahidi kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo na adhima ya Serikali ya kuondoa umasikini kwa watanzania na kuinua uchumi wa Taifa kwa ujumla.

 Katika mahafali hayo jumla ya vijana 106 wavulana 54 na wasichana 52 walihitimu mafunzo hayo ya ufundi wilayani Ikungi.


Share To:

Post A Comment: