Mwenyekiti na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji, Yona Mwambeta, akihubiri Jumapili wakati akiongoza harambee kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la Moraviani Usharika wa Kijichi jijini Dar es Salaam.
Waumini wa kanisa hilo wakiwa katika ibada hiyo.
Ibada ikiendelea.
Ibada ikiendelea.
Mwenyekiti na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji, Yona Mwambeta (kushoto) na Mchungaji wa kanisa hilo Usharika wa Kijichi, Raphael Mwampagatwa wakiwa kwenye ibada hiyo.
Maombi yakiendelea.
Harambee ikiendelea. Kushoto ni mke wa Mwenyekiti na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji, Yona Mwambeta, Mchungaji Lilian Mwambeta akihesabu sh.550.000 walizotoa kama mchango wao wa ujenzi wa kanisa hilo.
Mchungaji Lilian Mwambeta, akimkabidhi fedha hizo Mwenyekiti wa harambe hiyo, Subilaga Mwambeta.
Waumini wa kanisa hilo na wachungaji wao wakiwa nje baada ya kuhitimisha harambee hiyo.


Na Dotto Mwaibale


MWENYEKITI na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini,  Mchungaji, Yona Mwambeta amelitaka kanisa hilo kutoridhika na badala yake waige makanisa mengine yaliyopiga hatua ya maendeleo kwa kujenga makanisa makubwa na kuanzisha miradi ya maendeleo nchini.

Mwambeta aliyasema hayo Jumapili wakati akiongoza harambee kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la Moraviani Usharika wa Kijichi jijini Dar es Salaam.

"Wamoravian tangu siku nyingi wao ni watu wa kuridhika na vitu vidogo nawaambieni badilikeni na kuiga wanavyofanya wenzetu wa makanisa mengine ambao wapo mbali kimaendeleo" alisema Mwambeta.

Alisema kazi ya ujenzi wa kanisa hilo si ya waumini wa kanisa hilo pekee bali ni ya Mungu hivyo uchache wao usiwakatishe tamaa ya kupata fedha za kujenga kanisa hilo.

Akitolea mfano kanisa la Itungi lililopo wilaya ya Kyela mkoani Mbeya alisema lilianza kujengwa na watu wachache lakini leo hii limekuwa ni kanisa la mfano.

Mwambeta aliwataka waumini hao wa Kanisa la Moravian Kijichi kujenga kanisa kubwa litakalo akisi miaka  100 ijayo bila kujali litachukua muda gani kukamilika ujenzi wake.

Aidha Mwambeta aliwataka waumini wa kanisa hilo kuwashirikisha watu mbalimbali bila ya kujali dini zao na madhehebu wanayotoka ili kulijenga kanisa la usharika huo.

Mwenyekiti wa ujenzi wa kanisa hilo Jackson Mwaisemba alisema harambee hiyo ni ya pili  na kuwa wataendelea kufanya nyingine ili kufikia malengo ya kupata sh.milioni 100 zitakazo saidia kuanza ujenzi wa kanisa  hilo.

Mchungaji wa kanisa hilo Usharika wa Kijichi, Raphael Mwampagatwa alimshukuru Mwambeta kwa kuendesha harambee na kuwapa ari na moto mpya waumini wa kuchangia ujenzi huo.

Mchungaji Mwampagatwa alitumia harambee hiyo kutoa namba ya Voda 5312023 na Tigo 0679-607003 kwa ajili ya makanisa mbalimbali, taasisi, mashirika, wafanya biashara na mtu yeyote ambaye atapenda kuchangia ujenzi wa kanisa hilo kiasi chochote cha fedha awe Dar es Salaam na maeneo mengine ndani na nje ya Tanzania na Mungu atawabariki.

Katika harambee hiyo fedha taslimu zilizopatikana zilikuwa ni sh.3,717,000, ahadi sh.4,685,000 na jumla ikiwa ni sh. 8,402,000.

Share To:

Post A Comment: