Na John Walter-Manyara
Katika
kuhakikisha bidhaa bandia zinadhibitiwa
nchini, Tume ya Ushindani (FCC), imepanga
kuyafikia makundi yote maalum kwa njia ya kuwapatia Elimu ya Utambuzi wa bidhaa
hizo ili kuepuka kuzitumia.
Hayo
yameelezwa na Mkurugenzi wa Udhibiti Bidhaa bandia tume
ya Ushindani, Godfrey Gabriel Mshana kwenye Semina ya watu 50 wenye Ulemavu wa wa Kusikia, iliyofanyika
Mjini Babati leo Septemba 17,2020.
Mshana amesema sambamba na elimu hiyo kwa kundi la
Viziwi, njia nyingine wanayoitumia ni kuzuia soko la bidhaa hizo ambazo hazijathibitishwa
na Mamlaka husika.
Mshana
amesema bidhaa bandia ni changamoto na zinamwathiri kila mmoja na vita dhidi ya bidhaa hizo ni mtambuka
hivyo jamii itoe ushirikiano na
tume ipo tayari kwa ajili ya kupokea
malalamiko muda wowote au kituo cha polisi.
“Vita ya
bidhaa bandia ni Mtambuka, athari ya bidhaa bandia haichagui hivyo tunahimiza ushirikiano kwa jamii nzima”
alisema Mshana
Ameeleza kuwa
Sheria ya alama za bidhaa ni sheria ya Jinai ambapo mtuhumiwa wa makosa hayo anaingia
kwenye kesi ya uhujumu uchumi ambapo adhabu yake ni Kifungo au faini, kuharibu bidhaa hizo na kuwafidia walioathirika.
Amesema Watu
ambao wamebainika kujihusisha na makosa
mbalimbali katika bidhaa ni watu 635 kwa
mwaka wa fedha uliopita ambao walikuwa wakiingiza bidhaa hizo bandarini huku katika masoko wakiwa wafanyabiashara wakubwa zaidi ya 300 katika
masoko mbalimbali nchini.
Wametoa elimu
hiyo kwa kundi hilo maalum la watu wenye ulemavu wa kusikia ikiwa ni mpango wa
tume kuhakikisha kwamba wanayafikia makundi yote ya aina hiyo ili kuwapatia mbinu ya kutambua bidhaa feki.
Tume
inafikisha elimu hiyo kwa wahusika kwa kutumia wataalamu wa kutafsiri lugha ya alama ambayo ni rahisi kuwafikia
walengwa.
Akifungua semina
hiyo Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Joseph Mkirikiti, alisema licha ya
kuipongeza tume hiyo kwa kazi kubwa inayoifanya hasa kuyapa elimu makundi ya
watu wenye ulemavu lakini alitaka utaratibu huo kuigwa na taasisi, mashirika na
watu wengine.
Mkirikiti amesema
watu wanaojihusisha na bidhaa bandia wanahitaji kupata faida kubwa ambapo watu
wa aina hiyo sio wazalendo wa nchi hii na wanakwepa kodi.
Post A Comment: