Vifaa tiba vilivyotolewa na mfanyabiashara kutoka China, JackMa kwa ajili ya kupambana na virusi vya Corona nchini Tanzania vimewasili usiku wa kuamkia leo Machi 25, 2020, na ndege ya shirika la Ethiopia.

Katika taarifa yake aliyoiandika kupitia ukurasa wake wa  Twitter Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, amemshukuru mfanyabiashara huyo pamoja na Serikali ya China kwa ujumla.

"Jana usiku sisi Tanzania tulipokea mchango wa vifaa tiba, ambavyo vitasaidia katika mapambano yetu dhidi ya COVID-19, shukrani zetu za dhati kwa mfanyabiashara JackMa na taasisi yake ya AlibabaGroup na Serikali ya Ethiopia" Ameandika Waziri Ummy.

Vifaa hivyo ni barakoa 100,000, vipimo 20,000, na mavazi ya kujilinda (protective suits) 1,000.

Last night we (Tanzania🇹🇿)received a donation of medical materials that will help in our fight against . Our gratitude and appreciation to China's @JackMa, @AlibabaGroup and the government of Ethiopia @AbiyAhmedAli.🙏@MagufuliJP @MsigwaGerson @TZMsemajiMkuu @TZEmbassy
View image on TwitterView image on TwitterView image on TwitterView image on Twitter
Share To:

msumbanews

Post A Comment: