Mfanyabiashara maarufu Jijini Arusha na kada wa chama chamapinduzi Ccm Philemon Mollel amewataka wanawake wa mkoa arusha kujitokeza katika nafasi mbali mbali za kugombea nafasi za uwongozi lengo kuimarisha jinsia  zote kuwa sawa. 

Akizungumza katika kongamano la wanawake katika kanisa la victory church Dokta Philemon amesema wanawake wanatakiwa kujitambua hasa kujikita katika siasa kama Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan , Naibu Spika Tulia Ackson pamoja na viongozi wengine. 

Dkt Philemon amesema lengo la 50 kwa kina baba na kina mama nikuona wanakua viongozi wote kama wakina baba wanavyo jitosa katika sekta mbalimbali za uongozi hapa nchini.


Share To:

msumbanews

Post A Comment: