Mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM Taifa Arif Abri akiwa viongozi wa jumuiya za CCM wilaya ya Iringa vijijini
JUMUIYA ya wazazi wa chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Iringa vijijni mkoani Iringa imepongeza jitihada mbali mbali zinazofanywa na mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM Taifa anayewakilisha wilaya ya Iringa vijijini Arif Abri katika kuiwezesha jumuiya hiyo kuwa na miradi yake.
Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Marco Kihongo alisema kuwa pamoja na misaada mbali mbali anayotoa maeneo mengine ndani ya jama na jamii pia Abri amekuwa hachagui kusaidia .
Alisema kwa upande wa jumuiya hiyo pamoja na misaada mingine amepata kuchangia pesa kiasi cha shilingi milioni 1 kwa ajili ya kutekeleza ahadi yake aliyoitoa kwa jumuiya hiyo ya kuchangia pesa hizo kwa ajili ya ununuzi wa kadi za jumuiya kwa wanachama wapya.
Alisema kwa upande wa jumuiya hiyo pamoja na misaada mingine amepata kuchangia pesa kiasi cha shilingi milioni 1 kwa ajili ya kutekeleza ahadi yake aliyoitoa kwa jumuiya hiyo ya kuchangia pesa hizo kwa ajili ya ununuzi wa kadi za jumuiya kwa wanachama wapya.
Kihongo alisema kuwa mchango huo wa fedha ni mtaji mkubwa kwa jumuiya hiyo kuweza kuongeza idadi kubwa zaidi ya wanachama wake na kuwa zoezi la uongezaji wanachama litaanza mara moja kuanzia sasa .
Katibu wa mbunge wa jimbo la Ismani ,Wiliam Lukuvi alisema kuwa jitihada kubwa zimekuwa zikifanywa na Arif Abri katika wilaya ya Iringa ni mfano wa kuigwa na kuwa kazi mbali mbali amekuwa akichangia hivyo kuchangia fedha hiyo ni mwendelezo wa misaada mbali mbali ambayo amekuwa akitoa.
" Tunaamini Mungu humjalia zaidi yule anayetoa kwa ajili ya wengine kifupi tunashukuru sana kwa misaada mbali mbali ya kijamii na chama katika wilaya ya Iringa vijijini " alisema Thom
Arif alisema wajibu wake ni kujenga chama na kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano chini ya CCM na ataendelea kufanya hivyo .
" nimeendelea kusaidia jumuiya zote na hivi karibuni wakati namtafuta katibu wa jumuiya ya wazazi nilimpigia mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM)wilaya ya Iringa vijijini ambae pia aliomba kusaidia pikipiki nilimuahidi kuwa asiwe na hofu nitampa pikipiki hiyo na nimewakabidhi tayari " alisema Arif
Post A Comment: