Mwenyekiti mpya wa Miomboni katika  Halmashauri ya Mji wa Babati Mathias Zebedayo ameahidi kufanya mambo makubwa ya kimaendeleo  MWANDISHI JOHN WALTER ANARIPOTI TOKA BABATI

Mwenyekiti huyo ni miongoni  mwa wenyeviti wa  chama Cha Mapinduzi (CCM) waliopita bila Kupingwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika  Novemba 24,mwaka huu.

Zebedayo  ameahidi kushughulikia kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wake ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa huduma ya umeme, Miundo mbinu ya Bara bara inayounganisha mitaa mbalimbali na kuwaweka wananchi pamoja bila kujali tofauti za itikadi  za vyama kwa kuwa lengo ni kuleta maendeleo.

Kwa kipindi cha  uongozi wake katika mtaa huo muhula uliopita, amemueleza mwandishi wa habari hizi kuwa amefanikiwa kurudisha eneo la shule ya msingi Miomboni lililokuwa limevamiwa na watu kinyemela,kwa kumwandikia barua waziri wa ardhi, nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi.

Mwenyekiti huyo amesema ujenzi wa shule ya msingi Miomboni utaanza muda wowote kwa nguvu za wananchi ili kuwaondolea adha watoto kwenda umbali mrefu kufuata shule.
Share To:

Francis Godwin Mzee wa matukiodaima

Post A Comment: