Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula akizungumza
Mwakilishi wa Makatibu Tawala wa Mikoa katika kikao hicho Mhandisi Zena Said
Na WAMJW - Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula amewataka
Makatibu Tawala nchini kuendelea kuzisimamia Hospitali za rufaa za mikoa
ambazo kwa sasa zinasimamiwa na Wizara ya Afya.
Dkt. Chaula amesema hayo leo alipokutana na Makatibu Tawala
kutoka Mikoa ya Tanzania Bara katika Kikao Kazi cha Viongozi wa
Hospitali za Rufaa za Mikoa kinachoendela kufanyika katika ukumbi wa
Chuo cha mipango Jijini Dodoma.
“Licha ya Hospitali hizi kuhamishiwa usimamizi kutoka Ofisi
ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) lakini bado
zipo kwenye maeneo yenu, tunawategemea nyie Makatibu Tawala kuzisimamia
hospitali hizi.” Amesema Dkt Chaula.
Dkt. Chaula amesema kuwa ni dhahiri lengo lilikuwa ni jema
tuu kutoka kwa Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli, kwamba Hospitali
zisimamiwe na Wizara ya Afya ili ziweze kuwa na mahusiano ya moja kwa
moja na Wizara ya Afya ambayo ndiyo Wizara mama inayotunga Sera na
Miongozo pamoja na kusimamia Wadau.
Naye Mwakilishi wa Makatibu Tawala wa Mikoa katika kikao
hicho Bi. Zena Said amempongeza Katibu Mkuu Wizara ya Afya kwa kuandaa
kikao hicho cha kihistoria ambacho hakijawahi kufanyika kabla.
“Hili ni jambo la busara, pamoja na kwamba hizi Hospitali
zimeondolewa kwenye mamlaka za Tawala za Mikoa lakini bado kuna mambo
mengi ambayo bado tunayafanya kwa niaba ya Wizara” amesema Bi. Zena na
kuendelea “Sisi kama viongozi tupo mikoani hatuwezi kukaa kuangalia
mambo yakiharibika tukisema hizi Hospitali sio za kwetu”
Bi. Zena Said amesema kuwa Bado wanawajibika kwa njia moja au nyingine kuzisimamia kwa ajili ya kuleta ustawi kwa wananchi.
Kikao hicho cha kihistoria kinafanyika kwa mara ya kwanza tangu kuhamishiwa kwa usimamizi wa Hospitali za Rufaa za Mikoa tarehe 25, Novemba 2017 ambacho kitakuwa endelevu kila mwaka huku kikiwakutanisha viongozi wa hospitali, Waganga wakuu wa Mikoa pamoja na watendaji na wadau wa Sekta ya Afya nchini.
Kikao hicho cha kihistoria kinafanyika kwa mara ya kwanza tangu kuhamishiwa kwa usimamizi wa Hospitali za Rufaa za Mikoa tarehe 25, Novemba 2017 ambacho kitakuwa endelevu kila mwaka huku kikiwakutanisha viongozi wa hospitali, Waganga wakuu wa Mikoa pamoja na watendaji na wadau wa Sekta ya Afya nchini.
Mwisho
Post A Comment: