Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk Maximilian Chuhula akizungumza wakati wa uzinduzi wa kitabu kinachoelezea changamoto na matarajio ya utangamano wa Afrika, mgogoro wa Sahara uliofanyika Chuo Kikuu cha Katoliki Ruaha (RUCU).
Kitabu kikizinduliwa 
Mhadhiri wa UDSM, James Zotto akielezea kuhusu kitabu kilicho zinduliwa

Mwandishi wetu, Iringa


Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Maxmilian Chuhula amewataka wasomi wa vyuo vikuu kutoogopa kufanya tafiti nje ya nchi ili mbali ya kuongeza maarifa, wazijue tabia za watu wengine kwenye mataifa yao.


Dk Chuhula ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Historia Tanzania, amesema hayo wakati wa uzinduzi wa kitabu kinachohusu matarajio ya utengamo wa Afrika, mgogoro wa Sahara katika ukumbi wa Chuo Kikuu Katoliki Ruaha (RUCU).


Kitabu hicho kilicho chapishwa na Africa Proper Education Network (APE), kimeandikwa na Dk Maxmilian akishirikiana na mhadhiri mwingine wa UDSM, James Zotto.

“Fanyeni tafiti nje ya Tanzania mjifunze vitu vingi, mjifunze kuhusu watu wengine wa Afrika na muongeze maarifa,” amesema na kuongeza;


“Kitabu hiki kinao uhalisia na naamini mkikisoma kitawaongezea maarifa ya kutosha kuhusu utengamano wa Afrika hasa mgogoro wa Sahara Magharibi,” amesema.


Alisema kitabu hicho kitakuwa  miongoni mwa vitabu vitakavyo wapatia wanafunzi uelewa mpaka kuhusu masuala ya utengamano waAfrika, hasa mgogoro wa Sahara Magharibi.


Dk Chukula alisema licha ya kuwa na maandiko mengi, kitabu hicho ni cha kwanza  kwenye safari yao kitaaluma.


Awali Zotto alisema uzinduzi wa kitabu hicho pia unamuenzi Profesa Gaudence Mpangala aliyekuwa  kati ya wasomi  wachambuzi mahiri kwenye masual ya kisiasa akifundisha RUCU mpaka mauti ilipomfika Februari 4, 2021.


“ Profesa Mpangala ni kati ya wahadhiri walio mjenga kitaaluma hasa katika masuala ya historia na migogoro, alinisimamia na kumuenzi, tukaona tuje kuzindulia kitabu kwenye chuo hiki,” amesema Zotto.


Mwandishi mwingine wa kitabu hicho, Dk Chuhula ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Historia Tanzania amesema hakuna ubishi kwamba, ili kuandika vitabu wanafunzi lazima wajikite katika kufanya tafiti.


Awali, Kaimu Mkuu RUDU, DK Makungu Bulayi aliwataka wanafunzi kujenga tabia ya kusoma vitabu na kujikita katika uandishi ili kufikia malengo yao kitaaluma.


Alisema uzinduzi wa kitabu hicho umekiheshimisha chuo chao hasa wakati huu wa utandawazi ambao, wanafunzi wanapaswa kujifunza mambo mengi Zaidi kwa kusoma vitabu vilivyoandikwa na wanazuoni tofauti.


Baadhi ya wanafunzi wa RUCU, walisema ujio wa kitabu hicho chuoni kwao utawapa mwanga mpana hasa wale waliojikita kwenye masuala ya historia.


“Tumepata mwanga mkubwa sana kwa ujio wa kitabu hiki Zaidi, tumejifunza kwamba tunaweza kufanya tafiti hata nje ya Tanzania,” amesema Daud Daud, mwanafunzi wa RUCU.


Mwisho.


 

WASHINDI 56 Promosheni ya Mtoko wa Kibingwa msimu wa 07 kuitazama Derby ya Kariakoo kati Simba na Yanga itakayofanyika kesho kwenye uwanja wa Mkapa Jijini DaresSalaam.


Akizungumza na Wanahabari mapema Leo Aprili 19,2024 Afisa Habari wa Kampuni ya Betika Tanzania Juvenalius Rugambwa wakati akiwapokea Washindi Promosheni ya Mtoko wa Kibingwa Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julias Nyerere amesema washindi hao wamepatikana kupitia droo ya mtoko Kibingwa iliyoanza Mapema Februari 2024.


"Kama mnavyowaona hawa ni washindi ambao wamepatikana kupitia kampeni yetu ya mtoko kibingwa,na hawa washindi waliowasili Leo wataenda kuungana na wenzao wa Dar es Salaam nakukamilisha idadi kamili ya washindi 56 na wote watakwenda kulala kwenye hoteli yenye hadhi ya nyota tano wakifatiwa na bata la Mbagala zakiem kushuhudia burudani ya Muziki wa Bongofleva itakayodondoshwa na chino Wana Man,Mczo,platform, sholo Mwamba na wengine kibao."


.Jevenalius ameongeza kuwa Msimu huu wa mtoko wa kibingwa umekuwa wa kipekee zaidi kwani promosheni yote kulikua na ongezeko la zawadi kwa wki pamoja na mwezi ambapo wametoa zawadi za simu aina ya smartphone pamoja na Android kwa washindi mbalimbali mbali na zawadi kubwa ya kushinda tiketi ya kushuhudia derby yenyewe.


Pia amesema washindi watapelekwa na Ving'ora kwenye kuitazama Deby ya Simba na Yanga na watakaa jukwaa la VIP .


Hata hivyo Jevenalius amesema kampuni ya Betika imekuwa ikitoa ushindi hapo hapo pia itaendelea kuonesha nia yao ya dhati kunyanyua michezo kuanzia mpira wa soko hadi kutoa udhamini katika michezo mbalimbali.


"Kama ambavyo tulivyo sisi mshindi akishinda anapewa zawadi zake hapohapo kwa haraka,tunawaomba watu waendelee kutupia ubashiri kwa kutembelea kwenye website yetu hata hii mechi ya Simba na Yanga ipo hapo"Amesema


Kwa upande wake Balozi wa Kampeni ya Mtoko wa Kibingwa Baraka Mpenja amesema hii miongoni mwa derby inayowakutanisha watu kutoka Mataifa mbalimbali hivyo kwa washindi hao wanaenda kuandika historia mpya katika maisha yao na ndio dhamira ya Kampuni ya Betika kuhakikisha inawapa nafasi wateja wake .


Aidha amesema anawatakia mchezo mzuri timu zote mbili huku akiwapa moyo washindi hao kuwa watashuhudia mechi hiyo Kifahari zaidi (VIP).


Nao baadhi ya washindi hao,akiwemo Musa John kutoka Mkoa wa Tabora akiwa shabiki wa Simba ameishukuru kampuni ya Betika kupata fursa ya kuitazama Deby ya Kariakoo kwani ilikuwa ndoto yake kuona wachezaji wa timu hiyo.


"Kweli Betika hawana longolongo ,kwa mara ya kwanza nimepanda ndege hata nilipoambiwa nimeshinda sikuamini nilikua Shambani lakini baada ya siku kadhaa kunitafuta kwa mara ya pili na kunijulisha niwatumie vielelezo vyangu ili wanifanyie utaratibu wa safari ya kuja Dar niliamini hivyo nawashukuru sana Betika "


Kutembelea zaidi jinsi ya kubashiri Piga *149*16# au zama www.betika.co.tz.

 


Waziri wa Madini Anthony Mavunde amefanya kikao cha pamoja na  Kampuni ya Perseus ya Australia ikiongozwa na Mtendaji Mkuu wake Ndg. Jaffer Quartamaine juu ya uendelezwaji wa mradi wa Nyanzaga unaomilikiwa kwa ubia kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Ore Corp ambayo hisa zake zimenunuliwa na Kampuni ya Perseus.

Katika Mkutano huo Waziri Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa kufanikiwa kukamilisha wa mchakato wa ununuzi wa hisa za Kampuni ya Ore Corp na kuitaka Kampuni hiyo kukamilisha kwa uharaka malipo ya fidia kwa wananchi wanaopisha mradi.

Pia Waziri Mavunde amewataka wawekezaji hao kuhakikisha wanaanza mapema uendelezaji wa mradi kwa mujibu ya makubaliano ya awali ya kimkataba ili nchi ianze kunufaika na matunda ya utekelezaji wa mradi huu mkubwa wa dhahabu katika Wilaya ya Sengerema,Mkoa wa Mwanza.

Akizungumza katika kikao hicho,Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Perseus Bw. Jaffer Quartamaine ameishukuru serikali ya Tanzania kwa ushirikiano mkubwa wakati wote wa mchakato wa ununuzi wa hisa za Kampuni ya Ore Corp na kuahidi kwamba wamejipanga kuanza uendelezaji wa mradi huu mapema kadri iwezekanavyo kutokana na mpangilio wa utekelezaji wa shughuli mbalimbali za utekelezaji wa mradi.

Ameongeza pia kwamba wamejipanga kufanya uwekezaji mkubwa na wa mfano kwa kutumia Teknolojia ya kisasa ili kuongeza uzalishaji wa dhahabu nchini.







Na Dickson Mnzava, Same.


Mahakama ya Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro imemhukumu kifungo cha miaka 20 jela Said Ramadhani Mshana miaka 45 mpare mfanyabiashara na mkazi wa masandare wilayani Same Mkoani Kilimanjaro baada ya kutiwa hatiani kwa makosa mawili ya kijangili.


Miongoni mwa makosa ambayo amekutwa nayo mshitakiwa huyo ni pamoja na kukamatwa na nyara za serikali kinyume cha sheria na kujihusisha na ujangili wa nyara za serikali.


Akitoa hukumu hiyo tarehe 18 April 2024 hakimu mkazi Mkuu mahakama ya Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro mheshimiwa Chrisanta Chitanda amesema mshitakiwa alikamatwa katika eneo la kandoto Kata ya kisima wilayani Same Mkoani Kilimanjaro akiwa na meno 6 ya tembo yenye uzito wa kg 33 na thamani yake ni 105,255,000 pesa za kitanzania sawa na USD 45000.


Awali mwendesha mashitaka wa hifadhi za Taifa Nchini (TANAPA)Ndugu Samweli Magoko amesema mnamo tarehe 28/02/2023 katika eneo la kandoto Kata ya kisima wilayani Same mshitakiwa alikamatwa na maafisa wanyama pori baada ya kumuwekea mtego mshitakiwa kuwa wao wananunua meno ya tembo ndipo mtu huyo alipo jitokeza na kusema anauza meno hayo ya tembo.


Magoko aliiomba mahakama hiyo ya wilayani Same kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa huyo ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hizo kwani makosa aliyotenda mshitakiwa huyo kwa mujibu wa sheria ni makosa ya kuhuju uchumi na yanafubaza jitihada za serikali katika kulinda na kuhifadhi rasilimali za Nchi kwa manufaa ya watanzania wote.


Kufuatia ushahidi huo ulitolewa na jamuhuri mahakamani hapo dhidi ya mshitakiwa huyo mahakama iliweza kumkuta na hatia ya kuhujumu uchumi na kosa la ujangili bwana Said Ramadhani Mshana hivyo hakimu mkazi mkuu mheshimiwa Chrisanta Chitanda kumhukum kwenda jela miaka 20 kwa kosa la kwanza la kukutwa na nyara za serikali kinyume na kifungu cha sheria namba 86(1)(2)(c) sura ya 283 marejeo ya mwaka 2022 sheria ya uhifadhi wa wanyama pori.


Mshitakiwa huyo pia amekutwa na kosa la pili la kujihusisha na nyara za serikali kinyume na kifungu cha 84(1) cha sheria ya uhifadhi wanyama pori sura ya 283 marejeo ya mwaka 2022 hivyo mahakama hiyo kumhukum tena mshitakiwa huyo kwenda jela miaka 20 ambapo adhabu hizo atazitumikia kwa wakati mmoja.


Mshitakiwa amekutwa na kesi ya kuhujumu uchumi namba 5/2023 shauri la uhujumu uchumi Na.5/2023.


Akizungumza nje ya mahakama hiyo Mkuu wa Uhifadhi Hifadhi ya Taifa Mkomazi Kamishina msaidizi wa uhifadhi Emmanuel Moirana ametoa rai kwa wananchi wote wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu wa namna hii kuacha mara moja kwani jeshi la uhifadhi kupitia kitengo cha intelejesia na upelelezi vimejipanga kukabiliana na uhalifu wowote wa nyara unaotokea ndani na nje ya Hifadhi.


Moirana amesema uhalifu wa namna hii unadidimiza jitihada za mheshimiwa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan za kukuza utalii Nchini.