Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Jiji la Arusha katika uwanja wa Shekhe Amri Abeid ambapo amewataka vijana kutambua kuwa anawahangaikia kwani wao Ni nguvu kazi ya Taifa.
Rais wa jamburi ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemuagiza mkuu wa wa mkoa wa Arusha John Mongela kwenda
wilaya ya Ngorongoro kuangalia tofati zilizopo Kati ya wananch
wanaoishi ndani ya hifadhi na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ili
kuangalia namna ya kutatua
Mhe.Rais alisema
kuwa huko awali kulikuwa na migogoro mingi Sana, kwani vijiji vingi
vimeingia kwenye hifadhi ,lakini wakaangalia migogoro hiyo kwa undani
zaidi ya vijiji 100 wameamua kuviacha vilipo, kwani wakivihamisha hakuna
pa kuvipeleka
Aidha alimshukuru Leigwanani Kisongo kwa
kumwambia kwamba Serikali ikikaa pamoja na wafugaji wanaoishi ndani ya
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, mgogoro huo utatatulika,hivyo Rais
wameahidi kumtuma mkuu wa mkoa kutafuta Suluhu.
"Vijiji zaidi ya Mia moja tumeviacha vibakie vilipo ,tukiviahamisha hatuna pa kuvipeleka,Ila nakushukuru Sana Leigwanani Kisongo kwamba
umetuambia tukikaa na sisi mgogoro utatatuta,nataka nikuahidi namleta
mkuu wa mkoa aje kukaa na ninyi yakimshinda nitaingia mwenyewe" Alisema
Rais.
Wakati huohuo Mhe.Rais amempa miezi 3 Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya karatu Rajabu Karia Magara kuhakikisha anakamilisha ujenzi wa hospital hiyo ili kumaliza tatizo la wqgonjwa kukosa huduma ya matubabu
Karatu Kuna hospitali ya wilaya ambayo imeanzwa kujengwa kuanzia mwaka
2019 fedha yote umetolewa ipo pale iqna hospitali haijaisha, nakupa
miezi mitatu kwasababu fedha yote unayo sioni kwanini hospital haijaisha
Ina mwaka wa pili Sasa haijaisha"Alisema Mhe.Samia
Amemtaka
kuhakikisha kuwa hospitali hiyo inamalizika kwa muda alioutoa ili
akienda Karatu nikute imemalizika nije niifungie na wannachi wapate
huduma
tukiviahamisha hatuna mahali pa kuvipeleka
Akizungumza
juu ya ujenzi wa Stendi Jiji la Arusha Mhe.Rais Alisema kuwa hlmshauri
Jiji ipeleke mchoro kwani Serikali inamradi wanaandaa wa kuomba fedha
hivyo zikipatikana watazileta kwaajili ya ujenzi wa Stendi hiyo
Kuhusu
suala la machinga. Alisema kuwa hawawezi kuruhusu sir za mjini
kuharibiwa Ila utatafutwa utaratibu Maalum ili kuhakikisha wanpatiwa
maeneo ya kufanya biashara zao
Kuhusiana
na masuala ya mikopo kwaajili ya kuinua uchumi alisema kuwa mikopo
yenye masharti nafuu kwaajili ya manufaa ya Taifa ataiileta Ila mikopo
kichefuchefu hatoweza kunichukua kwasababu inawasogeza watanzania
inaleta Maendeleo hivyo hataogopa kuichukua
“Nataka
kuwaahidi watanzania nitaangalia mikopo yenye unafuu kwa nchi yetu,
inayoleta faida kwa nchi yetu hiyo nitaichukua, mikopo chechefu
sitaichukua lakini ile ambayo inaleta nafuu kwa nchi yetu, inatusogeza
watanzania inaleta maendeleo hiyo sitaogopa nitaichukua,”- Rais Samia
Suluhu Hassan.
Post A Comment: