Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Jiji la Arusha katika uwanja wa Shekhe Amri Abeid ambapo amewataka vijana kutambua kuwa anawahangaikia kwani wao Ni nguvu kazi ya Taifa.



Rais wa jamburi ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemuagiza mkuu wa wa mkoa wa Arusha John Mongela kwenda wilaya ya Ngorongoro kuangalia tofati zilizopo Kati ya wananch wanaoishi  ndani ya hifadhi  na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ili kuangalia namna ya kutatua

Mhe.Rais alisema kuwa  huko awali kulikuwa na migogoro mingi Sana, kwani vijiji vingi vimeingia kwenye hifadhi ,lakini wakaangalia migogoro hiyo kwa undani zaidi ya vijiji 100 wameamua kuviacha vilipo, kwani wakivihamisha hakuna pa kuvipeleka

Aidha alimshukuru Leigwanani Kisongo kwa kumwambia kwamba Serikali ikikaa pamoja na wafugaji wanaoishi ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, mgogoro huo utatatulika,hivyo Rais wameahidi kumtuma mkuu wa mkoa kutafuta Suluhu.

"Vijiji zaidi ya Mia moja tumeviacha vibakie vilipo ,tukiviahamisha hatuna pa kuvipeleka,Ila nakushukuru Sana Leigwanani Kisongo kwamba umetuambia tukikaa na sisi mgogoro utatatuta,nataka nikuahidi namleta mkuu wa mkoa aje kukaa na ninyi yakimshinda nitaingia mwenyewe" Alisema Rais.

Wakati huohuo Mhe.Rais amempa miezi 3 Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya karatu Rajabu Karia Magara kuhakikisha anakamilisha  ujenzi wa hospital hiyo ili kumaliza tatizo la wqgonjwa kukosa huduma ya matubabu 

  Karatu Kuna hospitali ya wilaya ambayo imeanzwa kujengwa kuanzia mwaka 2019 fedha yote umetolewa ipo pale iqna hospitali haijaisha, nakupa miezi mitatu kwasababu fedha yote unayo sioni kwanini hospital haijaisha Ina mwaka wa pili Sasa haijaisha"Alisema Mhe.Samia

Amemtaka kuhakikisha kuwa  hospitali hiyo inamalizika kwa muda alioutoa ili akienda  Karatu nikute imemalizika nije niifungie na wannachi wapate huduma 
 tukiviahamisha hatuna mahali pa kuvipeleka

Akizungumza juu ya ujenzi wa Stendi Jiji la Arusha Mhe.Rais Alisema kuwa hlmshauri Jiji ipeleke mchoro kwani Serikali inamradi wanaandaa wa kuomba fedha hivyo zikipatikana watazileta kwaajili ya ujenzi wa Stendi hiyo

Kuhusu suala la machinga. Alisema kuwa hawawezi kuruhusu sir za mjini kuharibiwa Ila utatafutwa utaratibu Maalum ili kuhakikisha wanpatiwa maeneo ya kufanya biashara zao

Kuhusiana na masuala ya mikopo kwaajili ya kuinua uchumi alisema kuwa mikopo yenye masharti nafuu kwaajili ya manufaa ya Taifa ataiileta Ila mikopo kichefuchefu hatoweza kunichukua kwasababu inawasogeza watanzania inaleta Maendeleo hivyo hataogopa kuichukua

Nataka kuwaahidi watanzania nitaangalia mikopo yenye unafuu kwa nchi yetu, inayoleta faida kwa nchi yetu hiyo nitaichukua, mikopo chechefu sitaichukua lakini ile ambayo inaleta nafuu kwa nchi yetu, inatusogeza watanzania inaleta maendeleo hiyo sitaogopa nitaichukua,”- Rais Samia Suluhu Hassan.
Share To:

Teddy Kilanga

Post A Comment: