Mkuu
wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani akikagua nyaraka za
sehemu ya vifaa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Usinge wilayani
Kaliua.
Mkuu
wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani akielekea leo katika
ukaguzi wa vifaa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Usinge wilayani
Usinge.
Mkuu
wa Wilaya ya Kaliua Paul Matiko akitoa maelezo ya awali kabla ya
kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani ambaye
alikuwa na ziara ya utekelezaji wa wa agizo la Waziri Mkuu alilotaka
uchunguzi wa matumizi ya fedha katika Kituo cha Afya cha Usinge.
MKUU
wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani ametoa siku saba kwa
Kamati ya Uchunguzi iliyoundwa na Mkuu wa Wilaya wa Kaliua kutoa taarifa
ya matumizi ya zaidi milioni 600 zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa
Kituo cha Afya cha Usinge.
Alitaka taarifa hiyo kufuatia utata
kwenye maelezo ya maendeleo ya ujenzi yaliyotolewa kwa Wajumbe wa Kamati
ya Usalama ya Mkoa ile iliyotolewa kwa Waziri Mkuu hivi karibuni wakati
wa ziara yake wilayani Kaliua.
Balozi Dkt.Batilda alitoa kauli
hiyo leo wakati ziara ya kikazi wilayani Kaliua ili kutekeleza la agizo
la Waziri Mkuu alilotaka uchunguzi wa matumizi ya fedha katika Kituo cha
Afya cha Usinge.
Alisema katika taarifa ya awali iliyotolewa na
Mtendaji wa Kata ya Usinge kwa Kamati ya Usalama ya Mkoa iliyoonyesha
uwepo wa akiba ya kiasi cha shilingi milioni 250 .
Balozi Dkt.
Batilda alisema katika taarifa ya Kurugenzi Mtendaji kwa Waziri Mkuu
ilionyesha kuwa wameshatumia kiasi cha zaidi milioni 600 na majengo
bado hayajaisha.
Alisema baada ya taarifa hiyo kama kutakuwepo
ma ubadhirifu wa matumizi ya fedha katika mradi huo watakaobainika
watachukuliwa hatua ikiwemo kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Awali
Mkurugenzi Mtendaji Jerry Mwaga alisema katika taarifa waliyotoa kwa
Waziri Mkuu hawakuweka gharama za vifaa ambavyo vilivyokuwa kuwa katika
ghala.
Alisema kuwa hali hiyo ilifanya kuonekana kuwa fedha zilizotumika ni nyingi kuliko hali halisi.
Naye
Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Paul Matiko alisema Kamati ya Uchunguzi
inahusisha Ofisi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU),
Ofisi ya Mkaguzi wa Ndani, Wahandisi wa Wilaya wa Wakala wa Maji na
Usafi wa Mazingira(RUWASA),Wakala wa Barabara Vijijini(TARURA) na Ofisi
ya UsalamaWilaya(DSO)
Wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kasim
Majaliwa katika Kituo hicho hakuridhishwa na matumizi ya fedha na kazi
ambayo imekwisha fanyika na kutoa miezi miwili kuhakikisha wamekamisha
bila hata kuongeza fedha nje ya walizopatiwa.
Fedha hizo zilitolewa kwa ajili ya Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD), Wagonjwa wa Ndani(IPD) na Upasuaji na Jengo la Wazazi.
Post A Comment: