Raisa Said,Bumbuli
WAKUU
wa Wilaya za Korogwe na Lushoto wamechukua hatua kadhaa kuzima mgogoro
wa ardhi uliokuwa unafukuta katika kijiji cha Kwebamba katika maeneo
ambayo yanasemekana yamegunduliwa madini aina ya silicon.
Wakuu
hao, Kalisti Lazaro wa Lushoto na Basila Mwanukuzi wa Korogwe walitoa
maamuzi hayo baada yakikao cha Ujirani mwema kilichofanyika katika
Kitongoji cha Kwebamba,lilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya
Bumbuli kufuatia taarifa za wananchi kumtaka Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, kuingilia kati mgogoro wa ardhi
unazingonganisha Halmashauri mbili za mkoa wa Tanga juu ya umiliki wa
eneo ambalo linasemekana limegunduliwa madini ya aina ya silicon.
Akitangaza
maamuzi hayo, Mkuu wa Wilaya ya Lushoto alisisitiza kuwa wakuu wa
wilaya hawakwenda kubadilisha mipaka kwa mujibu wa Tangazo la serikali.
“Sisi
kama wakuu wa Wilaya tumekuja kufanya maamuzi ili muendelee kuishi kwa
amani. Kila kitu kina mamlaka yake. Sasa haya ya serikali, wakurugenzi
na wakuu wa idara na Halmashauri zote mbili za wilaya watakaa vikao
kuzungumzia suala hilo na kufanya mapendekezo, kama watabadilisha GN kwa
vikao halali au watabdilisha ramani hiyo ni kazi ya wataalamu,”
alisema.
Alisema kuwa wameamua shughuli za kiutawala za kijiji
hicho ziendelee kama ioivyolues chini ya Halmashauri ya Bumbuli hadi
hapo hatua za kubadilisha Tangazo la serikali la Mwaka 1963 lililounda
mipaka ya wilaya zitakapochukuliwa.
Tangazo hilo kwa mujibu wa
Lazaro liliweka eneo hilo katika wilaya ya Korogwe wakati ambapo ramani
inaonyesha liko katika wilaya ya Lushoto
“sisi kama viongozi
tumetumia busara ifuatayo vingozi wa Bumba na wananchi wa kijiji hicho
na vitongoji vyake, kwa sasa, wanabaki kama ilivyokuwa kwa mujibu wa
uchaguzi ulivyofanyika. Hatuwezi kubadilisha sasa hivi. Vijiji kama
vijiji ni halali kwenye usajili, mgogoro uko katika Tangazo la Mwaka
1963 na mwaka 1948,” alisema.
Alisena kuwa kinachowagonganisha
vijiji vyote ni ugawaji wa mapori, ugawaji wa msitu na madini. Alipiga
marufuku kwa serikali za kijiji kujihusisha na ugawaji wa vitalu vya
uchimbaji. “Suala la ugawaji wa vitalu vya kuchimba madini wa utoaji wa
vibali ni mamlaka husika ambayo ni Ofisi ya Madini,” alisema.
Alifafanua
kuwa kazi ya Halmashauri husika ni kusimamia namna ya uchimbaji sio
kugawa wala kitoa leseni. “Eneo likishakuwa na maliasili kijiji hakina
mamlak. Suala kugawa eneo la machimbo,na kutoa leseni ni mamlaka husika
ambao ni Ofisi ya Madini ya Mkoa,” alisema.
Akizungumzia kuhusu
ugawaji wa maeneo ya pori ambayo ambayo hayawana watu inabidi serikali
za kijiji ziwe na mpango wa matumizi bora ya ardhi ya kijiji. Alisema
ana taarifa kuwa vijiji husika, Mtoni Bombo na Bumba havina mipamgo
hiyo.
“Hivyo kuanza sasa hivi hakuna kijiji kinaruhusiwa kukaa
kikao na kugawa ardhi au kuuza ardhi na kuchukua ushuru hadi hapo
Mamlaka za Halmashauri za vijiji husika zitakapowasilisha mpango huo
katika muda wa siku 60 kuonyesha matumizi mbalimbali. Mkiendelea kugawa
na kuuza na kuchukua shilingi elfu tano tano mtaleta vita kwenye vijiji
vyetu.” Alisisitiza.
Lazaro alifafanua kuwa eneo la msitu siyo
mali ya vijiji, bali mali ya Wakala wa Misitu (TFS), hivyo ni marufuku
serikali za vijiji kukaa na kugawa maeneo hayo kwa sababu maeneo hayo
siyo ya kijiji chochote.
Alisema wameelekeza TFS wasimamie na
walinde maeneo yao yasivamiwe. Kama wameona hayafai tena kuwa msitu
watoe taarifa na kukabidjhi kwa mamlaka husika ili lipangiwe matumizi na
sio serikali za kijiji kugawa na hiyo ndiyo inaleta matatizo.
Naye
Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Basila Mwanukuzi alisisitiza kuwa wao kama
viongozi lengo lao ni kutenda haki lakini lazima Tanzania inaongozwa na
sheria ambazo zitawafanya wafanye maamuzi sahihi.
“Tumekaa muda
mrefu. Tumejadiliana, tumeshirikishana na wataalamu wa ardhi,
tumeangalia ramani, kila kitu tumeangalia, tumejadiliana kwa kina,
tumeshauriana ili tufanye maamuzi yaliyo sahihi kwa ajili ya wananchi
wetu wote,” alisema.
Kaimu Kamishna wa Ardhi Mkoa wa Tanga,
Shaabani Mruma, alisema mgogoro ulishawahi kushughulikiwa miaka ya nyuma
(2007) na Wizara ya Ardhi waishirikiana na Wilaya hizo mbili.
Alisema
walianza kuushughulikia mwaka 2018 na kimsingi waliangalia matangazo
yaliyounda wilaya hizo mbili na Halmashauri ya Bumbuli na kimsingi
matangazo yote ni halali kisheria.
Mruma alisema walifika katika
eneo husika walibaini kuwa kuna vijiji 4 ambavyo vinaingia katika
mgogoro ambavyo ni Kikumbi, Bumba, Kalalani na Mtoni Bombo
Hata
hivyo, alieleza kuwa vyote vimesajiliwa na Tamisemi lakini vilivyopimwa
ni viwili, Mtoni Bombo na Kalalani na vingine havijapimwa. “Inawezekana
havikupimwa makusudi pengine kutokana na mwingiliano wa matangazo ya
serikali,” alieleza.
Alisema kuwa kijiji cha Mtoni Bombo hakina
matatizo kiko ndani ya mipaka ya wilaya ya Korogwe. Kijiji Bumba, kwa
mujibu wa Tangazo la serikali kipo ndani ya mipaka ya Korogwe lakini
huduma zake zote kinapata kutoka Bumbuli kwa maana ya elimu, afya na
masuala ya uchaguzi.
Mruma alisema kuwa walichobaini ni kuwa
kulikuwa na migogoro inahusu ardhi wakigombea ugawaji wa ardhi katika
maeneo hayo. Kila kijiji kilikuwa kinadai haki ya kugawa ardhi.
Pia alisema kuwa walibaini kuwa Tangazo la Halmashauri halikuzingatia mipaka mama ya Wilaya ya Lushoto.
Post A Comment: