Wafanyakazi watano wa TRA wamefariki dunia kwa ajali ya gari mkoani Songwe alfajiri ya leo baada ya gari lao kuligonga Lori kwa nyuma.
Kamanda
wa polisi wa mkoa wa Songwe, Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa
ajali hiyo leo alfajiri katika barabara ya Mbeya Tunduma eneo la
Hanseketwa wilaya ya Mbozi mkoani Songwe.
Taarifa za awali
zinadai kuwa Watumishi hao walikuwa kazini, ambapo walikuwa wakitumia
gari hiyo kufukuza gari nyingine iliyohisiwa kubeba bidhaa za magendo.
Post A Comment: