Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi akizungumza leo Mkoani Morogoro.
Na Jackline Lolah Minja - Morogoro
Kiongozi
wa mbio za Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi amekataa kuweka
jiwe la msingi katika mradi wa vyumba vya madarasa shule ya sekondari
Mazimbu iliyopo katika Wilaya ya Morogoro mkoani Morogoro baada ya kuwa na mkanganyiko wa nyaraka zinazohusu shule hiyo.
Akizungumza
mara baada ya kukagua mradi wa majengo ya shule ya sekondari Mazimbu
leo Jumatano Agosti 10,2021 Luteni Josephine Mwambashi amesema hakuna
mchanganuo halisi wa fedha zilizotumika kujenga majengo ya madarasa hayo
yenye thamani ya shilingi milioni 65.
Aidha
kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru amemuagiza mkuu wa wilaya ya
Morogoro ,Albert Msando kuhakikisha anafuatilia nyaraka zote za mradi
huo.
Post A Comment: