Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru akitoa mada kuhusu mlipuko wa virusi vya UVIKO 19 kwenye mkutano wa wadau kuhusu masuala ya msaada wa kisheria .
MGANGA wa Hospitali ya Mount Meru Hospitali jijini Arusha Sunday
Wanyika ameeleza kuwa kufa na kuzaliwa kwa cell mara kwa mara kwa
watoto ndio sababu inayopelekea watoto kutoshambuliwa na Virusi vya
UVIKO 19 vinavyosababisha ugonjwa wa homa ya Mapafu.
Ametoa
maelekezo hayo jijini Arusha leo wakati akitoa mada Kuhusu mlipuko wa
Virusi vya UVIKO 19 kwenywe mkutano wa wadau Kuhusu masuala ya msaada wa
kisheria na upatikanaji haki kwa wananchi katika kipindi cha matumizi
ya lugha ya kiswahili.
Mganga huyo ameeleza kuwa hali hiyo ndio
imekuwa ikisababisha watoto kutoshambuliwa n Virusi hivyo mana
vinapotaka kushambulia vinakuta cell zimekufa na kuanza kuzalishwa
nyingine hivyo wao wakijikuta wanakuwa sugu na kuwa na uwezo wa kupokea
na kuambukiza na kuathiri watu wazima.
"Zaidi ya aslimia 50 ya
wagonjwa hawaonyeshi dalili na wanaongoza kwa kusambaza Virusi vya
ugonjw huo hivyo wakati wa kujikinga usiwahofia ambao wameshaugua na
kuonyesha dalili tu, muwe makini pia na kundi hilo, mpaka sasa
watubmilioni 199 wameshapimwa na kukutw na maambukizi huku watu milioni 4
wakifariki na ugonjwa huo ulimwenguni,"amesema.
Ametoa wito kwa
wananchi kuhakikisha wanakuwa makini kwa kujikinga na maambukizi ya
virusi hivyo kwa kuchukua tahadhari zote ikiwa ni pamoja na kuhakikisha
wanachoma chanjo ambalo ni lazima kutokana na hali halisi ilivyo sasa,
kutokwenda kwenye mikusanyiko isiyo ya lazima na kutulia majumbani,
kuvaa barakoa ambazo zinakinga, kutumia vitakasa mikono na kunawa maji
tiririka.
"Simu za mkononi zinaongoz kwa mambukizi kutokana n
kushikwa mara kwa Mara nawasii wannachi muwe nazo makini kw kutumia
vitakasa mikono mara kwa Mara,"amesisitiza.
Akizungumzia Virusi
vya UVIKO 19 awamu ya sasa amesema viko tofauti sana na vile vya awmu ya
kwanza vinasambaa kwa haraka zaidi na ni rahisi kusababisha kifo huku
akitaja dalili namba moja kuwa ni kifua kuuma na kuwa kizito wakati
awali ilikuwa ni kupta mfua, kukohoa na kushindwa kunusa.
Akifungua
mkutano huo Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Godfrey Mizengopinda
amewataka mawakala wa sheria kwenye maeneo yao wapambanie afya za watu
wao suala la chanjo ni muhimu Sana kwa maisha ya watanzania hivyo
amewaasha washiriki wote wajitokeze kuchoma chanjo katika zoezi la
uzinduzi wa changjo litakalofanyika kesho jijini Arusha ili kujikinga.
Post A Comment: