Kamanda  wa Polisi wa  Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa Kipolisi Kinondoni Notker Kilewa akizungumza na Madereva wa Daladala katika Kituo cha Mawasiliano jijini Dar es Salaam.



KIKOSI Cha Polisi cha Usalama Barabarani kimesema kuwa hakuna taarifa rasmi ya daladala kuwa idadi ya abiria kuendana na idadi viti (Level Seat.)

Askari akipata usumbufu wa Dereva kazi hiyo apewe aweze kuifanyia kazi kwani Mechi ngumu kazi kubwa ni kutoa Pasi ili mwingine aweze kucheza.

Akizungumza na Madereva na Abiria katika Kituo cha Daladala Mawasiliano Kamanda  wa Polisi wa Usalama Barabarani  Mkoa wa Kinondoni Notker Kilewa amesema kuwa taarifa hizo hutolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) au Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani na sio vinginevyo.

Amesema kuwa viongozi wa juu wakitangaza kinachofanyika ni  utekelezaji wa agizo hilo kuwa na level seat.

Amesema kuwa Daladala  mbovu hazitakiwi atakayekamatwa ni dereva pamoja na mmliki wa Daladala wote watawekwa ndani.

Kilewa amesema  dereva wa daladala akirudisha  Daladala mbovu kwa mmiliki, anajitokeza dereva mwingine kulitaka Daladala hiyo licha ya kuwa na ubovu akikamatwa  dereva atawekwa ndani kazi ya mmiliki kuchukua Daladala yake na kufanya matengenezo.

Aidha amewataka  Madereva na makondakta kuwa na ustaarabu wa kuvaa na kuoga kwani hakuna makosa yaliyoanishwa juu ya mtu aliyemchafu kuchukuliwa hatua.

Kilewa amezitaka Daladala zote katika Mkoa huo kuwa na Jacks Mwanga  sheria ambayo ilitungwa mwaka 2015 hivyo ni lazima itekelezwe.

Amewataka makondakta kuacha tabia ya kukimbilia Askari wa  Usalama  Barabarani pale anapokamatwa kwa kuwa ni  ni kosa, Askari anawajibu  wa kumfuata dereva wa gari na kusisitiza kuwa akiwakuta dereva na askari wote ndani.

Share To:

Post A Comment: