Na Mariane Mariane Mgombere, Busega-Simiyu.
Mkuu
wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria amezindua rasmi zoezi la
chanjo ya UVIKO 19 (COVID 19) Wilayani Busega, uzinduzi uliofanyika
Hospitali ya Wilaya ya Busega, huku akiwataka wananchi kupuuza maneno na
taarifa za kizushi zinazoendelea kusambaa kwenye baadhi ya Mitandao
kuhusu chanjo hiyo. Mhe. Zakaria amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi
kupata chanjo, kwani Serikali ina malengo mazuri katika kupambana na
ugonjwa huo.
Aidha,
Mhe. Zakaria amesema ni muhimu kwa wananchi kuendelea kuchukua
tahadhari ya ugonjwa huo ili kupunguza maambukizi ya UVIKO 19.
Kwa
upande wake Kaimu Mganga Mkuu Wilaya ya Busega, Dkt. Beatus Silas
amesema zoezi la chanjo ya UVIKO 19 imezinduliwa rasmi siku ya tarehe 05
Agosti 2021, na zoezi litaendelea mpaka tarehe 11 Agosti 2021, huku
akiwataka wananchi kujitokeza kwa wingi.
Nae,
mratibu wa chanjo Wilaya ya Busega Bw. Mussa Shaban amesema Wilaya
imepokea jumla ya chanjo 2875 na itatolewa katika vituo 3
vilivyoelekezwa na Wizara ya Afya, ambavyo ni Hospitali ya Wilaya, Kituo
cha Afya Lukungu na Kituo cha Afya Igalukilo, hivyo wananchi waendelee
kujitokeza kwaajili ya kupata chanjo hiyo.
Kwa
upande wa wananchi baada ya kupata chanjo hiyo wamesema waniashukuru
Seriakli kwa kuleta chanjo nchini na kusisitiza kwamba ni muhimu kwa
wananchi wengine kujitokeza kuchanja ili kuwa na kinga dhidi ya ugonjwa
huo, kwani chanjo hiyo haina utofauti na chanjo nyingine.
Post A Comment: