Na Magreth Katengu - Dar es salaam
Tanzania
inaendelea kupiga hatua kiuchumi na kiteknolojia hivyo Taasisi za fedha
hazina budi kuwasogezea wananchi huduma hizo karibu kwa njia ya
kidigital ili kuwasaidia kuokoa muda wanaotumia kutembea mwendo mrefu
kufuata huduma.
Hayo yamesemwa na mkuu wa kitengo cha masoko na mawasiliano Akiba Bank Dora Saria jijini Dar es salaam katika uzinduzi wa huduma ya wakala ijulikanayo kwa jina la Akiba Wakala ambapo amesema huduma hiyo itawasaidia wateja kupata huduma kwa urahisi popote pale walipo kupitia mtandao
Amesema
benki hiyo imekuwa mshiriki mzuri katika kuunga mkono harakati za
serikali za kuhakikisha uwepo wa huduma jumuishi za kifedha kwa
watanzania wote
"Tumeingia
sokoni na jumla ya wakala wapatao 200 na tunaendelea kukidhi kiu ya
upatikanaji wa huduma kufuata mteja potote alipo kwa kumpatia huduma
zetu ikiwemo Amana,mikopo,kutoa na kuweka fedha", alisema Dora
Kwa
upande mmoja wa wakala wa ACB Faidha kiiwiri amesema mchakato wa
kutumia huduma ya benki hiyo gharama zake utoaji pesa kupitia wakala
gharama zake ni nafuu zaidi kupitia kazi hiyo kama kijana amejiajiri na
maisha yake yamebadilika
Aidha
amewaomba watu wote wajiunge na benki hiyo kwani imekuwa mstari wa
mbele kusaidia na kuwainua watu wenye kipato cha chini kwa kuwakopesha
kwa riba nafuu ili wainue uchumi wao
Post A Comment: