Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongela,amewataka Wananchi wa Mkoa huo kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima sambamba na kuendelea kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa UVIKO-19 kwa kuvaa barakoa na kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka.
Mhe.Mongela
ameagiza hayo wakati wa ziara yake ya siku moja Wilayani Arumeru ya
kukagua mashamba ya mazao ya mbogamboga, maua, matunda na viungo kwa
lengo la kuona uhalisia wa uendeshaji wa mashamba hayo.
Aidha,
amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe.Samia Suluhu Hassan,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kuhakikisha sekta
zote za kiuchumi zinakuwa na tija.
Mhe.Mongela
amesema baada ya kutembelea mashamba hayo siku ya Kesho atakua na kikao
na wadau wa Kilimo cha mazao ya mbogamboga, matunda na maua ili
kuhakikisha sekta hiyo inafanya vizuri.
Post A Comment: