Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Dk. Batilda Burian akitoa hotuba kuzindua program ya yaraConnect ya Kampuni ya mbolea ya Yara, inayolenga katika kutoa elimu ya utaalamu wa kilimo katika hafla iliyofanyika mkoani humo jana. Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilata ya Tabora, Dk. Yahya Nawanda na Meneja Masuluhisho ya Kidigitali wa Kampuni ya Yara, Deodath Mtei. Progamu hiyo inapatikana katika simu janja kupitia programu za play store na app store.
Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Dk. Yahya Nawanda, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa program ya yaraConnect kwa Mkoa wa Dodoma jana. Programu hiyo inayopatikana kwenye simu janja kupitia ‘play store na app store’ inalenga katika kutoa elimu ya utaalamu wa masuala ya kilimo ilizinduliwa na Mkuu wa Mkoa huo, Balozi Dk. Batilda Burian (kushoto kwake
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Dk. Batilda Burian (kulia), akitambulishwa kwa baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Mbolea ya Yara na Bwanashamba Mauzo Kanda ya Ziwa na Magharibi wa kampuni hiyo, Khaji Halidi (kulia kwake), alipokwenda kuzindua program ya yaraConnect kwa Mkoa wa Dodoma jana. Programu hiyo inayopatikana katika simu janja kupitia ‘play store na app store’ inalenga katika kutoa elimu ya utaalamu wa masuala ya kilimo.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dk. Batilda Burian (wa pili kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Dk. Yahya Nawanda (kushoto), akiwa na baadhi ya maofisa wa Kampuni ya Mbolea ya Yara wakati wakiwasili kwa ajili ya uzinduzi wa program ya yaraConnect kwa mkoa wa Tabora jana. Programu hiyo inayopatikana katika simu janja kupitia ‘play store na app store’ inalenga katika kutoa elimu ya utaalamu wa masuala ya kilimo. Wa pili kushoto ni Meneja Masoko wa Yara, Sheila Chatto na Meneja Huduma kwa Wateja Kidigitali, Eva Sauwa. Baadhi ya mawakala na wauzaji wa mbolea ya Yara mkoani Tabora wakihudhuria uzinduzi wa programu ya yaraConnect kwa mkoa huo mjini humo jana. Programu hiyo inayolenga katika kutoa elimu ya kitaalamu katika masuala ya kilimo inapatikana katika simu janja kupitia programu za play store na app store.
 Meneja Masuluhisho wa Huduma za Kidigitali wa Kampuni ya Mbolea ya Yara, Deodath Mtei (katikati), akielekeza jinsi ya kujiunga na programu ya yaraConnect kwa baadhi ya mawakala wa mbolea ya yara wa Mkoani Tabora, wakati wa uzinduzi wa programu hiyo mkoani humu jana. Programu ya yaraConnect inapatikana kwenye simu janja kupitia ‘play store na app store’
Share To:

Post A Comment: