Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiwa sambamba na Meya wa Manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada wakikagua miradi ya maendeleo inajengwa katika halmashauri hiyo
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiwa sambamba na Meya wa Manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada wakikagua miradi ya maendeleo inajengwa katika halmashauri hiyo
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiwa sambamba na Meya wa Manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada wakikagua miradi ya maendeleo inajengwa katika halmashauri hiyo
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiwa sambamba na Meya wa Manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada wakikagua miradi ya maendeleo inajengwa katika halmashauri hiyo

Na Fredy Mgunda,Irnga.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo amesema kuwa wakandarasi watakao chelewesha au kujenga chini ya kiwango miradi ya kimaendeleo katika halmashauri ya Manispaa ya Iringa watarudia kwa gharama zao kwa ubora ule ule unatakiwa kutokana na thamani ya mradi husika.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miradi ya kimaendeleo katika manispaa ya Iringa, mkuu wa wilaya Mohamed Hassan Moyo alisema kuwa amefanikiwa kukagua miradi mingi ambayo imejengwa kwa viwango vinavyotakiwa ila tatizo kubwa lipo kwa wakandarasi ambao wamekuwa wakipewa tenda za ujenzi wa miradi hiyo.

alisema kuwa wakati wa ziara aligundua kuwa wakandarasi wengi wameshalipwa fedha serikali kwa ajili ya kutekeleza miradi ya serikali ila wamekuwa wanaichelewesha kwa makusudi na kusababisha kuchelewa kuanza kufanya kazi kwa miradi hiyo.

Moyo alisema kuwa miradi mingi ilijengwa kwenye halmashauri ya Manispaa ya Iringa imejengwa kwa ubora unatakiwa kulingana na thamani ya fedha iliyotakiwa kutumika katika mradi husika.

Alisema kuwa watendaji wa Manispaa ya Iringa wanatakiwa kusimamia vilivyo fedha ambazo zinakuwa zinatolewa kwa ajili ya miradi ya kimaendeleo ili kusaidia kuwa na miradi iliyojengwa kwa viwango bora.

Moyo aliwataka wananchi wa manispaa ya Iringa kuhakikisha wanatunza miundombinu ya miradi ambayo imejengwa kwenye mitaa yao ili kuhakikisha miradi hiyo inatoa manufaa ambayo yamekusudiwa na serikali ya kuchangia kukuza maendeleo.

Mkuu huyo wa wilaya ya Iringa alifanikiwa kutembelea mbalimbali kama vile kukagua ujenzi wa choo cha zahanati ya Kitanzini,kukagua shule ya msingi Azimio,ujenzi wa choo cha shule ya msingi chemchem,ujenzi wa jengo la zahanati ya Itamba,ujenzi wa maabara shule ya sekondari ya Mivinjeni,ujenzi wa madarasa manne ya shule ya msingi mawelewele,ujenzi wa shule ya sekondari ya Kwakilosa na kutembelea ujenzi wa madarasa mawili shule ya msingi Njia Panda.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada alisema kuwa wameyapokea maagizo yote yaliyotolewa na mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo na watayafanyia kazi ili kuondoa kasoro ambazo zimejitokeza kwenye baadhi ya miradi ambayo kamati hiyo wameitembelea.

Aliwataka watendaji wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa weledi unaotakiwa ili kutumia fedha za wananchi vizuri kuendana na mradi ambao unakuwa unatekelezwa kwenye maeneo yao.





Share To:

Post A Comment: