Angela Msimbira, DAR-ES-SALAAM


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  Prof. Riziki Shemdoe  amesema kuwa  shule ya Sekondari ya Kibasila ni miongoni mwa shule 86 zilizokarabatiwa  kupitia mradi wa lipa kulingana na Matokeo  unaolenga kuoboresha  mazingira ya kufundisha na kujifnzia kote nchini


Prof. Shemdoe ameyasema hayo leo kwenye hafla ya uzinduzi wa magari 184 kwa ajili ya ufuatiliaji katika shule za Msingi kwenye Halmashauri zote nchini  iliyofanyika katika shule ya sekondari ya kibasila Mkoani Dar es salaam.


Akifafanua kwanini walichagua uzinduzi wa magari ufanyiwe hapo amesema  kuwa shule ya Sekondari ya Kibasila ilijengwa  mwaka 1951 na kuanza kutumika kama sekondari mwaka 1979 na ni moja ya shule ambayo imekarabatiwa  kupitia mradi wa lipa kulingana na matokeo


Amefafanua kuwa  Lengo kuu la kuchagua eneo hilo ni kuonyesha juhudi kubwa iliyofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuboresha miundombinu ya shule ikiwemo ukarabati wa shule kongwe.


Amesema kuwa pia eneo  la uzinduzi limepambwa na mjasiriamali mmoja wa wanufaika wa  nikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Serikali katika Manispaa ya Temeke hii inaonyesha utekelezaji wa Sheria unaofanywa na Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kuhakikisha wananchi wanajikwamua kiuchumi.


Amesema  pamoja uzinduzi wa magari  pia kuna ukarabati wa shule umefanywa  kwa ajili ya kuhakikisha wanafunzi wa Kitanzania wanapata mazingira mazuri ya kujfunzia.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: