KatibuMtendajiwaTumeyavyuoVikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa (Kushoto) akipata maelezo ya utafiti wa matumizi ya Bundi kutoka kwa Prof. Loth Mulungu kutoka Kituo cha udhibiti wa viumbe waharibufu cha Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA alipotembelea banda la SUA kwenye maonesho na mashindano ya Kitaifa ya Sayansi teknolojia na Ubunifu MAKISATU 2021 kwenye Uwanja wa jamhuri Dodoma.
Mbunifu wa FARM ART kutoka SUA Mussa Dotto akitoa maelekezo kwa Waziri wa Mawasiliano na teknolojia ya habri Dkt. Faustine Ndugulile ( wapil ikulia) alipomtembelea Mbunifu huyo kwenye maonesho na mashindano ya Kitaifa ya Sayansi teknolojia na Ubunifu MAKISATU 2021 kwenye Uwanja wajamhuri Dodoma

1.       Katibu Mtendaji waTume ya vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa (Katikati) akipata maelezo ya utafiti wa Mende kutoka kwa Mkurugenzi wa Kituo cha Udhibiti wa viumbe waharibufu cha SUA Prof. Ladislaus Mnyone (wa kwanza kulia) na Kushoto ni Prof. Loth Mulungu.

1.       Wataalamu wa matumizi ya panya kwenye kugundua vimea vya TB na Kutambua mabomu wakitoa malezo na kufurahia jambo na Katibu Mtendaji wa Tume ya vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa kwenye banda la SUA kwenye maoneshoya MAKISATU 2021 jijini Dodoma .

1.       1.       Mhandisi Neema Sumari kutoka Idara ya mathematics, Informatics and computational Sciences akimweleza ubunifu wake  Katibu Mtendaji wa Tume ya vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa kwenye banda la SUA MAKISATU 2021  mfumo unaoitwa Geospatial based real time system for land use/land cover detection.

Waziri wa Mawasiliano na teknolojia ya habari Dkt. FaustineNdugulile akimsikiliza mbunifu kutoka SUA, Patrick Mpombeye ambaye anashiriki mashindano ya MAKISATU 2021 akionyesha teknolojia yake ya udhibiti wa panya kwenye mashamba ya mpunga ya wakulima.

1.       Afisa mawasiliano wa SACIDS Yunus Karashan akitoa malezo ya kazi za SACIDS na teknolojia ya AFYA DATA kwa Katibu Mtendaji wa Tume ya vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa.

Katibu Mtendaji wa Tume ya vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa akiwa ndani ya gari la maabara inayotembea akipata maelezo kutoka kwa mtaalamu wa SUA jinsi gari hilo linavyofanya kazi za kimaabara na vifaa vilivyomo.

 Katibu Mtendaji wa Tume ya vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa akiangalia uoto kwenye maji ya samaki wa mapambo kwenye banda la SUA kwenye maoneshoya MAKISATU 2021 jijini Dodoma.

Share To:

Post A Comment: