Na Issa Mtuwa – Kagera Stamigold
Wizara ya Madini imetoa kipindi cha miezi miwili kwa Mgodi wa STAMIGOLD kuwasilisha Mpango wa kuanzisha Migodi Mipya.
Kauli
hiyo kwa STAMIGOLD ambayo ni Kampuni Tanzu ya Shirika la Madini la
Taifa (STAMICO) inafuatia kuonyesha uwezo wa kuanzisha na kuendesha
migodi mipya.
Hayo
yamesemwa Novemba 21, 2020 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof.
Simon Msanjila alipotembelea mgodi huo wa STAMIGOLD unaomilikiwa na
Serikali kupitia STAMICO kwa lengo la kuona maendeleo ya uendeshaji wa
shuguli za mgodi huo.
Baada
ya kufika mgodini hapo, Meneja Mkuu wa Stamigold Mhandisi Kilasha
Shamika alitoa taarifa ya uendeshaji wa mgodi pamoja na changamoto
zinazojitokeza wakati wa uendeshaji wa mgodi.
“Leo
ninatoa agizo ndani ya miezi miwilikuanzia Desemba na Januari 2021
mwishoninataka nipatiwe taarifa hiyo inayoonesha mpango wa kuanzisha
Migodi Mipya,” alisisitiza Prof. Msanjila.
Baada
ya kufika mgodini hapo, Meneja Mkuu wa STAMIGOLD Mhandisi Kilasha
Shamika alitoa taarifa ya uendeshaji wa mgodi pamoja na changamoto zake
zinazojitokeza wakati wa uendeshaji wa mgodi.
Mhandisi
Shamika alimueleza Katibu Mkuu kuwa uendeshaji wa shuguli za mgodi
zinaendelea vizuri na hadi hivi sasa mgodi unajiendesha kwa fedha
zake.
Ameongeza
kuwa kutokana na uzalisha wanaoufanya, hawapati faida kubwa lakini
kiasi hicho kinawapa nafasi ya kupunguza madeni ya zamani ambapo mgodi
teyari umeshalipa shilingi bilioni kumi (Bil. 10) kati ya jumla bilioni
39 wanazodaiwa.
“Kutokana
na uendeshaji wa mgodi, mgodi kwa sasa hauzalishi madeni mapya. Mgodi
unatekeleza maagizo mbalimbali yaliyotolewa na viongozi katika utoaji wa
motisha kwa wafanyakazi”, alisema Mhandisi Shamika.
Aliongeza
kuwa katika kutekeleza kwa maagizo hayo, Mgodi umeanza kutowa mikataba
ya miaka miwili miwili ambayo inawapa utulivu kazini. Pamoja na hilo,
wafanyakazi wametafutiwa fursa ya kupata mkopo kutoka kwenye benki
mbalimbali na uanzishwaji wa chama cha wafanyakazi.
Akizungumzia
kuhusu changamoto Mhandisi Shamika alisema, suala la ukosefu wa umeme
ni tatizo na kueleza kwamba . gharama za mafuta zimekuwa kubwa ambapo
kila mwezi hutumika bilioni 1.2, wakati endapo wengetumia umeme gharama
yake ingekuwa Shilingi milioni 300 kwa mwezi na hivyo kuokoa kati ya
shilingi milioni 700 au 800 kwa mwezi.
Alisema changamoto nyingine ni mtaji kwa ajili ya kuanzia miradi mingene kama mradi wa Visusi.
Katika hatua nyingine, Prof. Msanjila alitoa pongezi kwa STAMIGOLD kwa kazi nzuri wanayoifanya mgodini hapo.
Aliongeza
kwa kuanza kuendesha mgodi kwa gharama zao, kutengeneza faida japo ni
kidogo, kulipa madeni ya zamani, kutoendelea kuzalisha madeni mapya na
kutengeneza mazingira ya utulivu kwa wafanyakazi.
“Nimefurahi
sanaa kwa haya yote mliyoyasema kwenye taarifa yenu. Nimefurahi
ingawaje mna changamoto kadhaa” alisema Prof. Msanjila.
Akizungumzia
changamoto zilizosemwa Prof. Msanjila alikiri suala gharama za mafuta
ni tatizo na kuahidi kulifuatilia suala hilo kwenye mamlaka zinazotakiwa
kuleta umeme mgodini.
Kuhusu mtaji alisema, Mgodi una asset ni pamoja la lesseni za uchimbaji ambayo ni sehemu ya mtaji.
Post A Comment: