****************************************

Dar es Salaam - Oktoba 14, 2020 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa mshindi wa Tatu kupata Tuzo za Taasisi zinazosimamia Biashara Duniani, 2020 (WTPO Awards 2020) katika kipengele cha matumizi bora ya ushirikiano (Best use of Patnership) katika huduma ya kliniki ya Biashara inayosimamiwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade)

Tuzo hizi zimetangazwa leo tarehe 14 Oktoba, 2020 jijini Geneva nchini Uswidi ambapo Tanzania imewakilishwa na Mhe Balozi Maimuna Kibenga Tarishi, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika ofisi za Umoja wa Mataifa- Geneva.

Tuzo hizo zinazosimamiwa na kutolewa na Kituo cha Biashara cha Kimataifa Duniani (ITC) ili kutambua michango ya Taasisi zinazosimamia sekta ya biashara duniani (TPO) katika kusaidia Wafanyabiashara wadogo na kati (SMEs) kuimarisha uzalishaji bora wa bidhaa zao, kuwajengea uwezo wa kufanya biashara na kuweza kuuza bidhaa wanazozalisha nje ya nchi.

Kwa mara ya kwanza Tanzania kupitia taasisi yake ya TanTrade imeweza kushiriki tuzo hizo katika kipengele cha matumizi bora ya ushirikiano kupitia huduma ya Kliniki ya Biashara kwa ushirikiano wa Benki ya Biashara ya Tanzania (NBC) ambapo huduma hii inalenga kutatua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara Wadogo, wa Kati na Wakubwa nchini baada ya serikali kuwa na andiko la Blue Print ili kujenga mazingira rafiki ya ufanyaji biashara na kuweza kufikia uchumi wa viwanda.

Tangu kuanzishwa kwake, huduma hii imepokea changamoto za wafanyabiashara 1,083 na kufanikiwa kutatua changamoto 229 na kero 705 zinashughulikiwa. Huduma imeweza kutolewa kwenye Maonesho 17 yaliyoratibiwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Zanzibar, Pwani, Geita, Singida, Simiyu na Arusha

Mashindano ya Tuzo hizo hutolewa kila baada ya miaka miwili ambapo Tanzania kwa mara ya kwanza amekuwa mshindi wa Tatu akitanguliwa na Uswidi na Viet Nam katika kipengele cha matumizi bora ya ushirikiano. Nchi nyingine zilizoshiirki katika kundi hilo ni Colombia, Misri, Uholanzi, na Zimbabwe ambazo ziliingia kwenye kwenye mchujo wa mwisho.

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: