Msaidizi wa Mufti Shehe Yusuph Hassani Tonge akizungumza na waandishi wa habari kuishukuru Taasisi ya Uturuki akiwemo Rais wao kwa msaada huo
 Watu wakiendelea na uchinjaji wa ngombe
 uchinjaji wa ngombe ukiendelea
 Wachinjaji wakiendelea kuchuna ngombe kama wanavyoonekana
 Mbuzi nao wakichunwa kwa ajili ya sikukuu
 Baadhi ya viongozi wa Taasisi za Kiislamu wakipatia ngombe ambao walitolewa kwao kwa ajili ya sikuuu ya Eid El Fitri

WATANZANIA wametakiwa kuendelea kuitunza amani iliyopo hapa nchini hasa wakati nchi ikielekea kwenye uchaguzi mkuu ambao utafanyika Octoba 28 mwaka huu uweze kufanyika kwa amani na salama

Wito huo ulitolewa na Msaidizi wa Mufti Shehe Yusuph Hassani Tonge Julai 31 mwaka huu wakati wa sikukuu ya Eid El Fitri mara baada ya kumalizika kwa zoezi la uchinjaji wa wanyama mbalimbali ikiwemo ngombe, mbuzi na kondoo.

Ikiwa ni zawadi kutoka kwa watu wa uturuki kwa ajili ya waislamu kupata sadaka ya kwendaa kusheherekea sikukuu hiyo ambayo ni maalumu kwa ajili ya uchinjaji.

“Tumekuja Tanga kuchukua wanyama ambao wametolewa na wafadhili mbalimbali kutoka nchini Uturuku wakiwemo wasilamu pamoja na Rais wao Recep Tayyıp Erdoğa hivyo tunashukuru sana kwa msaada huu na tunaomba mwenyezi mungu akijalia watuletee tena mwaka ujao”Alisema Msaidizi wa Mufti.

Shehe Tonge ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa ya Waislamu nchini alisema waislamu hutumia siku hiyo ya kuchinja kwa sababu ya kumbukumbu ya nabii Ibrahimu alipopewa amri ya kumchinja mwanaye na badae kuletewe kondoo.

Alisema hiyo ni ishara ya amani na kwa sababu watanzania wanaelekea kwenye uchaguzi mkuu tukio hilo la kutoa sadaka kwa mwenyezi mungu liisaidie nchi yetu kuingia kwenye uchaguzi mkuu wa amani na umalizike salama.


Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: