Mbunge aliyemaliza muda wake lakini pia amepita kwa kishindo katika kura za maoni zilizofanyika juzi katika jimbo la Itilima amemwelezea Marehemu Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa kuwa alikua ni mzalendo na amewasaidia mengi katika wilaya hiyo.

Mwanasiasa huyo Njalu Daudi amsema enzi za uhai wa Mkapa aliwasaidia kujenga jengo la upasuaji 'Theatre'  kwa kupitia taasisi anayoingoza ya Mkapa foundation.

"Alikua ni rafiki yangu  taifa limepoteza shujaa wa nchi na  nguzo ya Afrika tumuombee apumzike kwa amani aidha  kwetu katika kata ya Nkoma tulikua na tatizo la kutokua na chumba cha upasuaji yaani Theater Mkapa alihakikisha kupitia Mkapa foundation anatimiza ndoto za wananchi  wengi waishio Nkoma sasa wazazi na wananchi wanapata huduma zote vyema na katika sehemu salama alitumia zaidi ya million 270 ameacha alama maishani mwetu ‘’ alisema Silanga

Aliongeza kuwa katika utendaji wake na ndio kasi pia anayokwenda nayo Rais John Magufuli kuwasimamia wayonge na kufanya utekelezaji wa mambo mbalimbali ya msingi katika taifa.

Mwisho
Share To:

Post A Comment: