Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kuwa Shule, makanisa, misikiti, vilabu, vilabu vya usiku, maeneo ya kufanyia mazoezi na saluni za urembo zitaendelea kufungwa ili kuepuka maambukizi ya virusi vya corona.

Museveni amesema kuwa si rahisi kwa maeneo hayo kufuata masharti ya kutochangamana.

Amri ya kutotembea usiku
Rais Museveni pia amesema muda wa kuwa ndani ya nyumba utaendelea kuwa kuanzia saa moja usiku mpaka saa kumi na mbili kamili asubuhi kwa siku 21 zaidi.

Makanisa, vilabu vya pombe, vilabu vya usiku , maeneo ya kufanya mazoezi na sauna yataendelea kufungwa kwa siku 21, huku kufungua shule kwa wanafunzi wanaotarajiwa kufanya mitihani kukiwa kumeahirishwa wakisubiri kwa mwezi mmoja.

''Tumeamua kuahirisha kufunguliwa kwa shule kwa wanafunzi wanaotarajiwa kufanya mitihani kwa mwezi mmoja zaidi tukijiandaa zaidi na kutazama hali ilivyo''.Alisema

Wenye magari ya dalala wamemaliza miezi miwili na nusu bila kazi tangu marufuku ilipowekwa mwezi Machi.

'Kuanzia tarehe nne nitaruhusu kuanza tena kwa usafiri wa Umma wa mabasi , usafiri wa abiria wa treni na dalala kuchukua abiria idadi ya nusu''. Alisema Rais Museveni.

Viwanja vya ndege vitaendelea kufungwa pia magari binafsi hayataruhusiwa kufanya kazi katika maeneo ya mpakani

Viongozi wa dini mwishoni mwa Juma lililopita waliomba nyumba za ibada baada ya kuchukua hatua ya kufungua masoko , kilio ambacho hakijasikilizwa na kiongozi huyo akiwataka waumini waendelee kusali kwa njia za televisheni wakiwa katika nyumba zao.

Share To:

Post A Comment: