Wakuu wa Mikoa kote nchini wameagizwa kuwachukulia hatua wale wote watakaobainika kuuza sukari kwa shilingi 4500.

Waziri Mkuu Mhe.Kasim Majaliwa amesema hakuna sababu ya sukari kupanda bei kwani sukari ipo yakutosha, ilikuwa imepungua imeagizwa na imekwishaletwa.

Majaliwa ameyasema hayo leo Jumatano April 22, 2020 akiwa kwenye Maombezi ya kuombea Taifa dhidi ya ugonjwa huu yanayofanyika katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar 

“Wiki hii waumini wa kiislamu wanaanza mfungo wa Ramadhan hivyo natoa wito kwa wafanyabiashara kuhakikisha vyakula muhimu vinauzwa kwa bei ya kawaida, Wakuu wa Mikoa na Wilaya wafanye ukaguzi mara kwa mara kwenye masoko ili kuhakikisha bei ni ile ile.

"Hakuna sababu ya bei ya Sukari kupanda, Sukari ipo tena ya kutosha, ilikuwa imepungua imeagizwa na imekwishaletwa, nawaagiza Wakuu wa Mikoa yeyote atakayeuza Sukari kwa Shilingi 4500, chukueni hatua kali dhidi yake" Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: