Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila amewaonya wananchi wa mkoa huo wanaoaminisha vijana kuwa pombe kali inaweza kutibu virusi vya corona kuacha mara moja imani hizo potofu, na kuwataka kuendelea kujikinga kwa kutumia vitakasa mikono na kuepuka makundi mbalimbali.

Chalamila amezungumza mara baada ya kukabidhiwa vifaa maalum vya kunawia mikono vilivyobuniwa na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia (MUST) ili kusaidia makundi mbalimbali kujikinga dhidi ya janga hilo.

Kiongozi huyo amesema baadhi ya watu wanafanya utani kwa kutumia pombe kali kusafisha mikono yao badala ya kutumia vitakasa mikono maalum vilivyoundwa kwa kazi hiyo.

“Na wengine wameanza kunywa pombe, wanasema kuwa wakilewa hawawezi kupata corona [virusi], mnajidanganya,” amesema Chalamila huku akiwataka wananchi kufuata utaratibu unaotolewa na wataalamu wa afya.

Vifaa vilivyotolewa na chuo hicho vitawasaidia wananchi lakini pia vitawaepusha kushika sehemu ambapo mtu mwingine ameshika mfano wakati wa kufungua koki au kuminya sauti.

Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya ( MUST) leo kimemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe Albert Chalamila mashine ya kunawia mikono iliyotengenezwa na wanafunzi wa chuo hicho kwa ajili kusaidia juhudi za Mkoa katika kujikinga na virusi vya Corona (COVID-19)
View image on TwitterView image on Twitter
See Ofisi ya MKuu wa Mkoa Mbeya's other Tweets
Share To:

msumbanews

Post A Comment: