Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Serikali imesema Suala la uboreshaji wa utoaji wa Elimu hapa nchini   ni endelevu, ambalo litaendelea kutokana na  mabadiliko yanayotokea .

Hayo yamesemwa  April 3,2020  Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia  Mhe.William Ole       Nasha wakati akijibu  swali la mbunge wa viti maalum  Mhe.Zainab Athuman Katimba aliyehoji Je, Serikali ina mkakati gani wa kufanyia maboresho Mfumo wa Elimu Tanzania?

Katika majibu yake kwa njia ya Maandishi Naibu Waziri wa Elimu Mhe.William Ole Nasha amesema maboresho ya Elimu ni endelevu katika utegemezi wa nyanja za kiuchumi na kijamii, pamoja na ulinganisho wa maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Mhe.Nasha ameendelea kufafanua kuwa , suala  la uboreshaji wa mifumo ya elimu limekuwa likifanyika na hutegemea tathmini mbalimbali za kitaalamu zinazofanyika kwa nyakati tofauti ,Mfano elimu ya sekondari ya chini (O Level) kutambuliwa kuwa ni sehemu ya Elimumsingi  na inatolewa bila malipo ya ada.

 Aidha, katika elimu ya ualimu Mhe.Nasha amesema  serikali imeongeza miaka ya kumwandaa mwalimu wa elimu ya awali kutoka miaka 2 kuwa miaka 3.

Pamoja na mabadiliko hayo, Serikali imeendelea na uimarishaji wa elimu Tanzania  kuwa ya umahiri (Competence based) kutoka katika mfumo wa awali ambao ulimwandaa mhitimu kwa nadharia bila mafunzo kwa vitendo ya kutosha.

Pia Nasha amesema Uboreshaji huo  umefanyika sambamba na uimarishaji wa mitaala katika ngazi zote.

Katika kuboresha mfumo wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi, Serikali imeunda mabaraza ya ujuzi ya Kisekta ambayo yanakuwa kiungo kati ya Vyuo vya Elimu ya Ufundi na wadau, vikiwemo viwanda na waajiri ambapo  Mabaraza hayo yatahakikisha kuwa mitaala inayotumika inakidhi mahitaji ya wadau na soko la ajira.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: