Serikali imesema licha ya mipaka ya nchi kujifunga kutokana na janga la ugonjwa wa COVID 19,wageni wachache wanaoingia nchini wanapokelewa kwa mujibu na taratibu za kuingia nchini na kuhudumiwa kwa hadhi inayoendana na mahitaji ya Kimataifa kama ilivyo katika nchi nyingine yeyote duniani huku tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huo ikipewa kipaumbele.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Kanali Wilbert Augustine Ibuge ameyasema hayo alipofanya ziara katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kukagua na kujionea namna wageni kutoka mataifa mbalimbali wanavyopokelewa na hatua wanazopaswa kuzifuata kabla ya kuruhusiwa kuingia nchini.

Balozi Kanali Ibuge amesema licha ya ukweli kwamba kwa sasa wageni wanaoingia nchini ni wachache sana kutokana na mipaka kujifunga ni muhimu serikali kuhakikisha kuwa wale wachache wanaoingia wanafuata taratibu za nchi na kupewa utaratibu wa namna ya kujikinga na ugnjwa wa COVID 19 bila ya uwepo wa malalamiko kutoka kwa wageni hao.

Ameongeza kuwa ameridhishwa na hali ilivyo katika uwanja huo wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa kuwa hadhi wanayopewa wageni hao haina tofauti na hatua zinazochukuliwa katika mataifa mengine duniani na kwamba ni muhimu kufanya hivyo ili kuhakikisha usalama wa Taifa na raia wake kwa ujumla.

Amewataa watumishi wanaoendelea kutoa huduma katika uwanja huo kuchukua tahadhari ya kujikinga na COVID 19 huku wakitumia kauli nzuri wakati wa kutoa huduma.

Katika ziara hiyo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Kanali Wilbert Ibuge amekagua jengo la kwanza la uwanja huo na jengo jipya la tatu akiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya viwanja vya ndege TAA Mhandisi Julius Ndyamukama.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: