Na Heri  Shaaban

TAASISI ya amani    Islamic Foundation  yampongeza Rais John Magufuli kwa utendaji kazi wake na  kusimamia amani ya nchi.

Hayo yalisemwa Dar es Salaam leo na Mwenyekiti wa Taasisi ya  amani ya Tanzania Islamic Foundation Sadiki Godigodi, wakati wa kuzungumza  na waandishi  wa  habari   kuelezea  mazuri yaliyofanywa na Rais wa awamu ya tano John Magufuli ikiwemo kudumisha amani na mshikamano kwa watanzania.


" Taasisi yetu kwa kushirikiana na viongozi wa dini mbalimbali tunachukua fursa hii ya kumpongeza juhudi za serikali ya Rais Magufuli kudumisha amani pia inawaonya watu wasitoe taarifa za uzushi za kutekwa watu bila kufatilia katika vyombo vya usalama" aliema Sadiki.

Sadiki aliema nchi yetu inaongozwa na sheria  unapokuwa una shaka na jambo zipo mamlaka zimeundwa kwa ajili ya kufatilia  usitoe taarifa ambazo ujazifanyia utafiti kwani vitendo hivyo vya uzushi havijengi umoja bali vinatengeneza dhana  hasi miongoni mwetu kutoaminiana.


Said alisema tulizaliwa Tanzania tutazikwa Tanzania hivyo kila mmoja jukumu lake kubwa kulinda amani   vizazi vyetu visihukumiwe   kwa mambo yanayofanywa sasa kimsingi yataathiri maisha yao baadae.


Katika hatua nyingine wamempongeza Rais kwa hotuba nzuri aliyotoa  hivi karibuni Zanzibar wakati wa madhimisho ya miaka 56 ya Muungano.


 Aliwataka watanzania  kudumisha amani  nchi yoyote ikikosa amani akuna maendeleo   kama kuna matatizo aliwataka watanzania mutumia njia za kutatua changamoto bila kuathiri amani, upendo na mshikamano.

MWISHO
Share To:

msumbanews

Post A Comment: