Mratibu wa mradi wa vijana na jinsia (USID Boresha Afya )  Faith Dewasi akielezea kazi za mradi huo 
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela  akitoa hotuba yake  wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili 
Kaimu katibu tawala mkoa wa Iringa Lucas Kambelenje  akitoa TAKWIMU za hali halisi ya ukatili wa kijinsia mkoa wa Iringa 
Baadhi ya washiriki kutoka asasi mbali mbali wakiwa katika maadhimisho  hayo 

..................................................................

Wakati  takwimu  za  jeshi la   polisi zikieleza kuwa   watoto  657    wanawake  414 wanawake  414
 na  wanaume 41  kwa mwaka  huu 2019 mkoa  wa Iringa wamefanyiwa vitendo vya ukatili  wa  kijinsia  ,mradi wa wa  jinsia  na vijana  (USID Boresha Afya ) umepania  kuendelea  kutoa  elimu kwa  jamii ya  mkoa   huo ili  kupambana na vitendo vya ukatili  wa  kijinsia .

Akizungumza   wakati wa   kilele  cha maadhimisho ya  siku  16  za  kupinga  ukatili wa kijinsia  ulimwenguni   jana  katika  maadhimisho ya mkoa yaliyofanyika kimkoa   katika kijiji  cha Kiwere  wilaya ya  Iringa mratibu  wa mradi   huo  Faith  Dewasi  alisema  kuwa  vitendo vya  ukatili  wa  kijinsia  ndani ya mkoa  wa Iringa vimezidi  kusika kasi jambo ambalo  ni hatari kwa ustawi  wa maendeleo ya  kiuchumi  katika mkoa  huo .

Hivyo  alisema   pamoja na  mradi  USAID Boresha  afya  upande  wa   jinsia na  vijana  umeendelea   kutoa  elimu  mbali mbali  kwa  makundi mbali mbali   ili  kusaidi   kupunguza  kama  si kumaliza  tatizo  la ukatili wa kijinsia  miongoni  mwa  jamii ya  wakazi wa  mkoa wa Iringa na kuwa kazi hiyo  imeendelea  kuwafikia watu  wengi   zaidi na sehemu  mabadiliko yameanza  kuonekana kwa jamii  kupaza sauti pale  wanapoona  vitendo vya ukatili  vinafanyika katika maeneo yao .

"  Ikumbukwe  kuwa  tupo  katika maadhimisho ya  kupinga ukatili duniani  na  sisi kama  shirika  ambao  tunapata  msaada  wa  fedha  kutoka kwa  watu  wa Marekani  tumeweza  kufanya kazi kubwa ndani ya  mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na  ofisi za  serikali  mkoa wa Iringa kwa  kuwafikia  wananchi  wa makundi mbali mbali  wakiwemo  walemavu ,walimu ,viongozi wa  serikali na makundi mengine  ili  kufikisha  elimu  hiyo " alisema 

Aidha  alisema   elimu  hiyo imekuwa  ikiwafikia  wataalam  mbali  mbali wakiwemo madaktari ,watu maarufu na  wengine  ili  kuonyesha  kuwa  suala la ukatili wa kijinsia  ni la makundi yote na  wote  wanahitaji kufiiwa na  elimu ya kupinga  ukatili wa  kijinsia  ili  kuweza  kukomesha  vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii  nzima .

Hata  hivyo alisema kutokana na elimu ambayo  wamepata kuitoa kwenye makundi mbali mbali  mbali na mahojiano  ambayo wameyafanya  kwenye makundi  hayo inaonyesha   suala la ukatili wa kijinsia katika mkoa wa Iringa linazungumzwa  kwa  zaidi ya asilimia 60 hali  inayoonyesha  kuwepo  kwa  uhitaji mkubwa wa   elimu ya kupinga  ukatili  kuendelea  kutolewa kwa jamii .

Dewasi  alisema mradi  huo wa Boresha  afya  umekuwa ukipiga vita  vitendo vya ubakaji  katika jamii   kwani  kumekuwepo na matukio mbali mengi ya ubakaji  ,ulawiti na utatili  mwingine kwa  watoto watoto  katika mkoa wa Iringa.

Alisema    kuwa asilimia  zaidi ya 80  ya  wanawake na  watoto ndani ya mkoa wa Iringa  wamekuwa wakifanyiwa   vitendo vya ukatili huku  wanaume ikiwa ni asilimia 10  wamekuwa wakifanyiwa ukatili wa  kijinsia  na wake  zao ila  wamekuwa  wakitunza  siri  kwa kutosema  popote .

Kuwa  wanaume  wengi  wamekuwa  wakifanyiwa ukatili wa kijinsia  ila  wamekuwa  hawasemi popote   kutokana na mila na desturi  walizonazo baadhi ya  wakazi wa  mkoa wa Iringa ambao   wamekuwa  wakiamini  kwenda  dawati la jinsia polisi  kulalamika kwa  kupigwa na mwanamke kwao ni aibu  jambo ambalo  si sahihi  kwani vitendo vya  ukatili wa kijinsia havitakiwi   kukumbatiwa kabisa kwa  mtu  yeyote  bila  kujali ni  mwanamke ama mwanaume  anatendewa  ukatili .

Alisema  kuendelea  kukumbatia  vitendo vya ukatili ama kuficha  siri  ya matukio  ya ukatili  yanapotokea ni  kuurudisha  nyuma mkoa na Taifa  katika  suala   zima  la  uzalishaji mali   na  kupelekea  manyanyaso kwa  watoto katika familia  kwani kama baba na mama wanatabia ya  kufanyiana  ukatili  suala la matunzo kwa  watoto   huwa  la  kiwango  cha chini zaidi  hivyo ni  vizuri  kila mmoja kupaza  sauti na wao kama mradi wa USAID Boresha afya  wataendelea   kutoa  elimu  dhidi ya  vitendo vya Ukatili wa kijinsia  .

Akitoa taarifa  ya hali ya  ukatili wa  kijinsia katika mkoa wa Iringa kwa  niaba ya katibu  tawala  mkoa Happines Seneda , katibu tawala msaidizi  mkoa wa Iringa Lucas Kambelenje  alisema   kuwa   hali ya  vitendo vya ukatili katika mkoa wa Iringa  inaendelea kuwa  kuwa ambapo  takwimu  zinaonyesha  kuwa  idadi ya  watoto ,wanawame na  wanaume  wanaofanyiwa  ukatili imezidi  kuwa kubwa  .

Alisema   kwa  mwaka 2018  watu  waliofanyiwa  ukatili  na kuripoti polisi  ni   watoto 406 ,wanawake 430 ,na wanaume 25  wakati  mwaka 2019  takwimu  ziliongezeka kwa kuwa  watoto  657    wanawake  414 na  wanaume 41.

Alisema  kuwa  ukatili  umekuwa  unafanyika  majumbani  ,njiani  wakati  watoto  wanakwenda  ama  kutoka   shule  na katika  kubaliana na tatizo hilo  jitihadfa  mbali  mbali  zinafanyika kwa  mwaka jana  2018  watuhumiwa  579  walikamatwa na  watuhumiwa 659  kwa  mwka 2019 walikamatwa  kati yao  watuhumiwa  64walitiwa  hatiani  mwaka 2018 na  mwaka 2019   watuhumiwa 25   walitiwa  hatiani kwa  kukutwa na makosa ya kufanya  vitendo mbali  mbali vya  ukatili  wa  kijinsia .

Kwa  upande  wake  mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi  ambae aliwakilishwa na mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela  katika maadhimisho  hayo  aliwataka  wananchi wa  mkoa wa Iringa  kuendelea   kuwafichua   wale  wote  wanaojihusisha na vitendo vya ukatili wa  kijinsia  ili  sheria 


iweze  kuchukua  mkondo  wake .

Alisema  kuwa  kwa  upande wa  wilaya ya Iringa umeanzisha  ushirikiano wa jeshi la zima moto na uokoaji  kwa  kutumia namba  ya  zimamoto 114  kwa wananchi  kupiga   simu  bure  ili  kufichua  matukio ya ukatili yanayofanyika katika maeneo yao .




Share To:

Francis Godwin Mzee wa matukiodaima

Post A Comment: