NA HERI SHAABAN(PWANI)


CHUO CHA Maendeleo  ya wananchi Kibaha chajivunia mafanikio  kwa kupanua wigo wa udahili wa wana chuo kutoka Mikoa yote Tanzania.


Hayo yalisemwa na Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha Joseph Nchimbi wakati wa mahafali  ya chuo hicho ambapo jumla ya wanachuo 142 wamehitimu kati yake wanawake 42 na wanaume 100.

" Chuo chetu cha KFDC kimepiga hatua kubwa katika kutoa mafunzo bora na kufanya vijana wengi kuomba nafasi katika chuo hiki ,kwa kipindi cha miaka mitatu kimeweza kudahili wanafunzi wengi na kufanya vizuri"  alisema Joseph

Joseph alisema mafanikio mengine ambayo wanajivunia wanachuo wote ambao wametoka katika chuo hicho wamepata ajira serikalini ,sekta binafsi na wengine wamejiari wenyewe sekta binafsi kutokana na ujuzi waliosomea chuoni ikiwemo ufundi umeme ,ufundi magari ufundi uchomeleaji na uundaji vyuma.


Aidha alisema idadi ya wakufunzi kila siku wanaongezeka waliohamia katika chuo hicho hivyo kupunguza uhaba wa wakufunzi waliokuwepo hapo awali wanaendelea kupata huduma bora kutoka kwa Wakufunzi wa Shirika la Elimu Kibaha.

Joseph alisema Chuo cha Maendeleo Kibaha (Kibaha Folk  Development College )kilianzishwa mwaka 1964  kikijulikana kama Farmers Training Centre  chini ya mradi wa pamoja wa serikali ya Tanganyika na nchi ya za Nordic uitwao  Tanganyika Nordic Project.

Alisema katika chuo  hicho kuna fani mbalimbali kwa ajili ya kujifunza  ikiwemo ufundi selemala,ufundi ushonaji,ufundi uashi,ufundi bomba,kilimo,mifugo na hotelia.


Joseph alisema chuo   hicho kinachangia nguvu  kazi muhimu inayohitajika katika uchumi wa viwanda uwezo wa chuo kuchukua wanachuo 500 lakini kwa sasa chuo kina wanafunzi 295 .


Kwa upande wake Mwanafunzi wa Chuo hicho cha Maendeleo ya Wananchi,Emanueli Leonard alisoma risala ya wanachuo wanaohitimu mwaka wa pili alielezea changamoto za chuo hicho ikiwemo uchakavu wa majengo,upungufu wa kompyuta,ukosefu wa jengo la kompyuta,uchakavu wa karakana za kujifunzia na ukosefu wa jengo la kujifunzia

Naye mgeni rasmi  Mjumbe wa Bodi wa shule hiyo   Elisante Joackim alipongeza Serikali kwa kuvitunza vyuo vya ufundi vilivyopo hapa nchini .

Elisante aliwataka wana chuo waliohitimu chuoni hapo watumie elimu waliopata kwa kujiongezea ajira na kuzingatia nidhamu kwani nidham ndio siri ya mafanikio  pia wajenge   umoja na  mshikamano .

Aliwataka vijana kuchangamkia fursa katika kukopa mikopo ya Serikali ambayo inatolewa ngazi ya halmashauri ya Wanawake Vijana na Watu Wenye ulemavu.

MWISHO
Share To:

msumbanews

Post A Comment: