Happy Lazaro,Arusha.
Makamu wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ,Samia Suluhu ametaka kuwepo kwa juhudi zaidi kwa ajili ya kuongezeka kwa idadi ya viongozi wanawake katika idara mbalimbali kuanzia ngazi za chini hadi juu ili kuendelea kuchochea maendeleo zaidi.
Ameyasema hayo leo wakati akifungua mkutano wa wabunge wanawake kutoka mabunge ya nchi za Afrika wanachama wa jumuiya ya madola unaofanyika jijini Arusha.
Samia amesema kuwa,kwa sasa hivi kuna mawaziri wanawake wapatao 7 kati ya mawaziri 23 na manaibu Waziri wanawake 4 kati ya manaibu 22,hivyo kufanya wawakilishi wanawake bungeni kufikia asilimia 24.4,hivyo kufanya takwimu hizi kuwa kubwa kuliko nchi zingine.
"pamoja na kuwepo kwa idadi hiyo ya wanawake viongozi bado juhudi zaidi zinatakiwa kuhakikisha kiwango hicho kinaongezeka na kufanya idadi hiyo kuwa juu zaidi katika ngazi mbalimbali."alisema.
Spika wa bunge la Tanzania ,George Ndugai akizungumza katika mkutano huo,alisema kuwa lengo kuu ni kutaka kuona kunakuwepo kwa uwiano sawa katika nafasi ya uongozi hasa kwa wanawake bungeni.
Hata hivyo alipongeza sana kuwepo kwa ongezeko la wanawake viongozi katika mabunge kwani uwepo wao unaleta mchango mkubwa sana na hamasa kwa wanawake wengine kuendelea kujitokeza kwa wingi katika nafasi hizo.
Ndugai aliongeza kuwa, kwa sasa hivi kuna asilimia 30 ya viongozi wanawake kuanzia ngazi ya serikali za vijiji,mitaa,majiji na hata wilaya ambapo ngazi zote zina wawakili kwa asilimia 30 ,ambapo alitaka juhudi zaidi kuendelea kuongezwa kuhakikisha wanawake wanaongezeka katika ngazi mbalimbali.
Kwa upande wa Mbunge wa Handeni Vijijini , ambaye ni mmoja wa washiriki Mboni Mhita alisema kuwa, dhana kuu ya mkutano huo ni kuangalia nafasi ya wanawake katika mchakato wa uchaguzi sambamba na kujadili changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika chaguzi mbalimbali na kuweza kuzipatia muafaka .
Mhita alisema kuwa,changamto kubwa iliyopo kwa wanawake kushindwa kushiriki nafasi mbalimbali ni kutokana na mfumo dume wa wanawake wengi kuona nafasi hizo ni za wanaume na hivyo wengi wao kujengewa na hofu na kushindwa kushiriki kikamilifu.
"napenda kuwasihi wanawake wote kuhakikisha wanajitoa sana katika kuwania nafasi mbalimbali za uongozi na kwa wale ambao wameshafanikiwa wahakikishe wanakuwa mabalozi wa kuwainua wanawake wengine."alisema .
Mwisho.
Post A Comment: