WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga(CCM) Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa ziara yake wa kukagua na kutembelea Hospitali ya wilaya ya Tanga na Kituo cha Afya cha Mwakidila Jijini Tanga kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya wa Wazazi wilaya ya Tanga Nassoro Makau
 WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga(CCM) Ummy Mwalimu kushoto akimsikiliza kwa umakini Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji mara baada ya kutembelea hospitali ya wilaya ya Tanga
 Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa ziara hiyo
 MKURUGENZI wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji akizungumza wakati wa ziara ya WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga(CCM) Ummy Mwalimu kulia kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Mkoba
 WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga(CCM) Ummy Mwalimu katikati akiwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kulia wakati wa ziara ya kutembelea hospitali ya wilaya ya Tanga inayojengwa eneo la Masiwani na kituo cha Afya Mwakidila
 WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga(CCM) Ummy Mwalimu katikati akiwa na wakazi wa Masiwani wakati wa ziara yake kutoka kushoto ni Mganga Jiji cha Tanga CMO
 WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu katikati akionyeshwa kitu na Mkurugenzi wa Jiji la Tanga daudi Mayeji wakati wa ziara yake
 Sehemu ya wananchi wa Masiwani wakiwemo wazee wakimsikiliza WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga(CCM) Ummy Mwalimu
 KATIBU Mwenezi wa CCM wilaya ya Tanga Lupakisyo Kapange kulia akicheza na wananchi wa Masiwani wakati wa ziara hiyo
 Muonekano wa mmoja ya majengo yaliyopo kwenye Hospitali ya wilaya ya Tanga eneo la Masiwani


 Muonekano wa mmoja ya majengo yaliyopo kwenye Hospitali ya wilaya ya Tanga eneo la Masiwani
 Muonekano wa mmoja ya majengo yaliyopo kwenye Hospitali ya wilaya ya Tanga eneo la Masiwani
 Muonekano wa Majengo kwenye Hospitali ya wilaya ya Tanga eneo la Masiwani Jijini Tanga

Muonekano wa mmoja ya majengo yaliyopo kwenye Hospitali ya wilaya ya Tanga eneo la Masiwani

WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Tanga inayojengwa eneo la Masiwani Kata ya Masiwani Jijini Tanga huku akitaka umaliziaji wake umalizika kwa wakati ili wananchi waanze kupata huduma za matibabu.

Kutokana na kazi nzuri iliyofanyika kwenye Hospitali hiyo ya wilaya Waziri huyo alimpongeza Mkurugenzi wa Halamshauri ya Jiji la Tanga Daudi Mayeji na wataalamu wengine akiwemo fundi ambao wanasimamia ujenzi huo kutokana na kujengwa kwa ufanisi mkubwa.

Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati alipofanya ziara ya kuitembelea na kukagua ujenzi wake unavyokwenda huku akionyesha kuridhishwa nao huku akimuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kuhakikisha vitu vidogo vidogo vya umaliziaji vifanyike kwa haraka.

Licha ya kutembelea hospitali hiyo lakini pia Waziri Ummy alitembelea pia ujenzi wa kituo cha Afya Mwakidila ambapo pia aliridhishwa na kasi yake huku akitaka kikamilika kwa wakati ili wananchi wa maeneo hayo wapata huduma hiyo muhimu.

Alisema kwani amepita sehemu mbalimbali Tanzania akiwa anakagua hospitali hizo huku baadhi akisema wabomboe kwenye baadhi ya maeneo kutokana na kujengwa chini ya kiwango lakini kwenye wilaya hiyo hajasema hivyo.

Waziri huyo aliwataka watumie miezi michache kumaliza kazi zilizobakia ili wananchi waanze kupata huduma hawana muda wa kusuburi hosipitali hiyo imesubiriwa kwa muda mrefu sana jiwe la msingi lililwekwa 2013.

“Maisha mangapi yamepotea kwa kukosa hospitali ya wilaya…wazee wangu na wananchi masiwani niwapongeze kutoka ndani ya moyo wangu kusimama kidete kuhakikisha kwamba hospitali inajengwa na kukamilika,tunawashukuru kwa uvumilivu kwa ushirikianao mkubwa wa kufika eneo hilo"Alisema

"Lakini pia mwenyezi mungu awazidishie heri mmetizima wajibu wenu kama wana Tanga na Tanzania maendeleo sio kama hayajaletwe yanaanza na sisi wenyewe jambo tunalosisitiza ni ushiriki wananchi katika kuleta maendeleo kwenye maeneo yao yanayowazunguka”Alisema

Aidha alisema kwamba wamekubaliana na Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Suleimani Jafo ndani ya muda mfupi huduma zianze kutolewa ili kuondosha kero za wananchi wa maeneo hayo.

Hata hivyo aliwaomba wakazi wa masiwani kuendeee kumuombea Rais Dkt John Magufuli heri na baraka kwenye suala zao kutokana na kazi kubwa na mapinduzi makubwa aliyoyafanya kwenye sekta mbalimbali hapa nchini ikiwemo za Afya

Awali akizungumza katika ziara hiyo Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa alisema kwamba huwezi kuzungunza jambo lolote la kuisifu nchi ukaacha kumtaja Rais Magufuli iwe sekta binafasi au umma kutokana na kufanya kazi kubwa ya kuwapa maendeleo watanzania.

Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji alisema kwamba ujenzi wa majengo saba kwenye hospitali hiyo yapo kwenye hatua umaliziaji na jengo ambalo limejengwa muda mrefu litajengwa litakuwa la utawala na wameweka utaratubu wa kutenga bajeti kulikarabati ili liweze kufafana na majengo mengine.

Alisema walipokea bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo na mpaka sasa wamekwisha kutumia zaidi ya bilioni 1.4 lakini kazi zote zinazohusiana na ujenzi huo wamewapa watu wanafanya ukamilishaji, milango, aluminiamu, watu wanaweka umeme, kazi zote na vifaa vyake zimekwisha kununuliwa.

Hata hivyo alisema kwamba mpaka sasa madaktari sita tayari wametengwa kwa ajili ya kuanzisha hospitali hiyo na wamekwisha kuandaliwa barua za kuhamishiwa kwenye hospitali hiyo.

Mwisho.
Share To:

Post A Comment: